Friday, September 30, 2011

Naibu waziri ahimiza Wahandisi Umwagiliaji, Wasaidie Kuibua Miradi ya Umwagiliaji

Naibu Waziri wa Kilimo chakula na Ushirika Mhe. Christopher Kajolo Chiza amewagiza Wahandisi wa Umwagiliaji, Kuwawezeshe wakulima kuibua miradi ya umwagiliaji.

Hayo aliyasema wakati akifungua mafunzo ya wiki mbili ya Wahandisi wa Umwagiliaji wa Umwagiliaji wa Kanda, Sekretariati za Mikoa na Halmashauri za wilaya, yaliyofanyika mjini Morogoro hivi karibuni

Mhe. Chiza aliagiza kuwa fedha zinazotolewa kwa ajili ya miradi ya umwagiliaji lazima zitumike kama zilivyokusudiwa.

Alisisitiza kuwa wakulima wajulishwe kiasi cha fedha kinachotumika katika miradi ya umwagiliaji, maana ya mifuko (Vyanzo vya fedha) ikiwa ni pamoja na umoja wao unaowawezesha kutekeleza vizuri miradi ya umwagiliaji.

Aidha Mhe. Chiza alisema kuwa serikali inalenga kuwa ifikapo mwaka 2015 asilimia 25 ya chakula chote kinachozalishwa nchini kitokane na kilimo cha Umwagiliaji, kwa kuongeza maeneo ya kilimo hicho kufikia hekta 1,000,000, na vile vile kulima kisasa katika maeneo yalioyopo

No comments:

Post a Comment