Wednesday, September 29, 2010

VIJANA WA TANZANIA NA SHILIKISHO LA AFRIKA MASHARIKI

Vijana wengi ukiwaambia watoe maoni yao kuhusu shirikisho la Afrika Mashariki, hulikosoa shirikisho hilo kwa nguvu ao zote. Wamekuwa na hofu juu ya ushindani mkubwa wa ajira na bidhaa wanazozalisha. Wengi wametoa maoni kwamba shirikisho lisilishwe ili wawe na uwezo wa kushindana na nchi nyingine wanachama.

Lakini hiyo ni hofu tu, vijana wengi hawana elimu ya kutosha kuhusu shirkisho la Afrika Mashariki, na wengi wamekuwa wakisubiri kuletewa taarifa na fursa zilizopo katika Jumuiya hiyo badala ya wao kutafuta taarifa na fursa zaidi walizo nazo.

Vijana tumekuwa tulitazama shirikisho kwa macho mawili ya kawaida hivyo tunaona matatizo mengi ndani yake. Tumeshindwa kutumia jicho la tatu kuona fursa tulizonazo sisi kama vijana wa kitanzania. Vijana wenzetu wa nchi nyingine hutafuta taarifa na fursa ndio maana tunaona wanafanikiwa na kufaidika katika shirikisho la Afrika Mashariki. Sifa kubwa ya kijana mjasiriamali ni kuona fursa wakati wengine wanaona tatizo, na fursa yoyote ile lazima iwe na changamoto zake. Changamoto huwa hatuzikimbii bali hinakabiliana nazo ili tupate matokeo mazuri.

Tanzania ukilinganisha na nchi nyingine wanachama wa Jumuiya, Tanzania imejaliwa kuwa na ardhi kubwa inayofaa kwa kilimo na kuweza kuwa mzalishaji na mlishaji wa Jumuiya Je, hiyo siyo fursa kwa kijana? Nchi zote haziwezi kuwa sawa kwa kila kitu kuna vitu ambavyo wenzetu wametuzidi na kuwa mambo mengi ambayo na sisi tumewazidi. Hamna sababu ya kupinga shirikisho wala kuomba muda mwingi zaidi wa kujiandaa. Kwani hata timu ya mpira ikijiandaa kwa muda mrefu bado itakumbana na ushindani mkubwa kutoka kwa wapinzani wao, mbinu kabambe zinahitajika wakati wa mchezo.

Vijana tukumbuke kwamba sasa tupo ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, hivyo tutambue changamoto zinazotukabili na kutafuta mbinu za kupambana na changamoto hizo. Vile kujifunza, kujikosoa na kuiga kile kilicho bora kutoka kwa wenzetu ambao tunaona wepiga hatua mbele. Hamna haja ya vijana kukaa na kupoteza muda kwa kupinga uwepo wa Jumuiya hii.

Ushiriki wa vijana wa Tanzania katika shughuli za mtangamano unawawezesha vijana kulinda maslahi ya Tanzania, na kufaidika na fursa zitokanazo na mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Vijana wanatakiwa kutafuta taarifa mbalimbali zinazohusu Jumuiya ili kupanua elimu waliyonayo kuhusu mtangamano wa Afrika ya Mashariki ikiwa pamoja na fursa zilizopo na jinsi ya kuzihimiza, lakini pia kuhusu changamoto zilizopo na jinsi ya kukabiliana nazo. Vijana tujiunge katika vikundi mbalimbali vya ujasiriamali ili kwa pamoja tuwezekushindana kikamilifu wa wafanyabiashara qa nchi nyingibe. Umakini, uhalali na ubora wa shughuli ambazo zifanywa na vijana wajasiriamali ni muhimu katika kuimili ushindani huo. Bidhaa zote tunazozalisha ni muhimu kuhakikisha bidhaa hizo zina ubora unaokidhi mahitaji ya soko ili kuvutia mlaji.

Yafuatayo ni maeneo ya msingi yanayohusishwa katika soko la pamoja, ambayo ni:-
a)Soko la uhakika kwa bidhaa mbalimbali, zikiwemo bidhaa za kilimo na viwanda katika jumuiya;
b)Uhuru wa raia wa Afrika Mashariki kusafiri katika nchi yoyote ndani ya Jumuiya(Free Movement of people)
c)Uhuru wa raia wa Afrika Mashariki kufanya kazi katika nchi yoyote ndani ya Jumuiya (Free Movement of workers);
d)Uhuru wa raia wa Afrika Mashariki kufanya biashara ya kudumu katika nchi yoyote ndani ya Jumuiya (Free Movement of servies); utekelezaji wa hatua hii unawahakikishia uhuru wa soko la biashara ya huduma katika sekta zilizofunguliwa na nchi wanachama kwa kuondoa vikwazo hatua kwa hatua, na kutoanzisha vikwazo vipya.
e)Uhuru wa raia wa Afrika Mashariki kuwekeza mitaji katika nchi yoyote ndani ya Jumuiya (Free Movement of Capital); utekelezaji wa hatua hii utawezesha kuondoa vikwazo kwa raia wa Afrika Mashariki kuwekeza kwenye soko la mitaji katika nchi nyingine ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki hatua kwa hatua kwa mujibu wa ratiba ya utekelezaji;
f)Haki ya raia wa Afrika Mashariki kuanzisha na kuendesha shughuli za biashara na uchumi katika nchi yoyote ndani ya Jumuiya (Right of Establishment); utekelezaji wa hatua hii unawahakikishia raia wa Afrika Mashariki haki ya kuanzisha na kuendesha shughuli za biashara na kiuchumi katika nchi yoyote Mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki bila ubaguzi kwa misingi ya utaifa au taratibu za uanzishaji kampuni hatua kwa hatua.
g)Aidha, Nchi wanachama zimekubaliana kuanzisha sheria na maeneo yanayolindwa kwa wananchi wa nchi husika na kuyawasilisha katika Baraza la mawaziri la jumuiya ya Afrika Mashariki ndani ya kipindi cha mwaka mmoja baada ya itifaki ya soko la pamoja kupata nguvu ya kisheria kwa lengo la kukubaliana jinsi ya kufungua maeneo hayo katika siku za usoni.
h)Haki ya ukazi kwa raia wa Afrika Mashariki katika nchi yoyote ndani ya Jumuiya (Right of Residence); utekelezaji wa haki hii unawawezesha raia wa nchi wanachama watakaopata ajira au kuanzisha shughuli za kiuchumi kuishi katika nchi yoyote mwanchama, kulingana na taratibu zilizokubalika.

Dira kuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ni kukuza kipato, kuinua hali ya maisha ya wananchi wa Afrika Mashariki, kukuza uchumi, na kujenga ushindani wa kanda katika ngazi ya kinataifa. Katika kutekeleza azma hii, nchi wanachama zinanufaika kutokana na mahusiano mazuri ya kibiashara na uwekezaji. Aidha nchi wanachama zinanufaika na progran kuendeleza mitandao ya barabara, reli, umeme, elimu, afya, usalama na utawala bora.

Kwa ujumla dira, malengo na mikakati ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ni nzuri endapo itafikiwa kwa wakati na walengwa kunufaika. Utekelezaji unahitaji uwajibikaji mkubwa wa Jumuiya serikari ya nchi husika na wananchi wake. Vijana wananafasi kubwa katika kutimiza malengo ya Juimuiya. Hivyo kila kijana anatakiwa atambue fursa na wajibu alionao katika jumuiya ili kuinua uchumi wake binafsi na wa Taifa kwa ujumla.

Na,
Innocent Mbele
Mwenyekiti mtendaji, FASO

Friday, September 24, 2010

WAJIBU WA VIJANA KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA

UTANGULIZI
Mapambano dhidi ya rushwa si ya Serikali au Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) peke yake bali ni ya jamii nzima. TAKUKURU ina jukumu la kuongoza na kushirikisha jamii nzima katika mapambano haya wakiwemo vijana. Kutokana na ukweli kwamba vijana ni rasilimali ya taifa, watendaji wa siku zijazo na chuchu ya mabadiliko katika jamii, wanao umuhimu wa kipekee kuleta mabadiliko ya kijamii hasa katika kubadili mtazamo wa jamii kuhusu rushwa kutoka kwenye matazamo kuwa rushwa ni sehemu ya utamaduni na jambo linalokubalika na kuiona rushwa kuwa ni kosa lisilotakiwa kuvumiliwa kwa namna yoyote kutokana na athari zake kwa jamii.

MAANA YA RUSHWA
Rushwa ni neno pana ambalo haliwezi kutosheleza na tafsiri moja japokuwa limekuwapo tangu zamani sana. Watu wengi wamejaribu kutafsiri rushwa katika mitazamo tofauti. Tunaweza kutafsiri rushwa kuwa ni:-
Kitu chochote cha thamani kinachotolewa au kupokelewa kinyume na sheria ili kupata au kutoa huduma.
Matumizi mabaya ya madaraka ya mtumishi wa umma ili kupipatia maslahi binafsi.

Rushwa hujumuisha kupindisha sheria, kanuni na taratibu za nchi kwa manufaa ya mtu binafsi na ya wale wanaopenda kutumia fedha au kitu chochote ili mtoe huduma afanye wanavyotaka wao.

SABABU ZA KUWEPO KWA RUSHWA
Kuna sababu mbalimbali zinazosababisha au zinazochangia kuwepo kwa rushwa ambazo ni:-
Mmomonyoko wa maadili miongoni mwa viongozi, watumishi wa umma na jamii kwa ujumla.
Elimu ndogo kwa wananchi juu ya haki na wajibu wao wa kupata huduma mbalimbali.
Ubinafsi na tabia ya uroho wa mali ili kujinufaisha na kujilimbikiza mali au utajiri.
Urasimu katika kutoa huduma mbalimbali.
Watu kutumia njia ya mkato kukamilisha na kutatua matatizo yao au kupata huduma.
Mishahara midogo kwa wafanyakazi wa serikali na taasisi zingine.
Watu wasio waadilifu kuchaguliwa au kuteuliwa kushika nyadhifa za juu na hivyo kusababisha kukosekana kwa utashi wa kisasa.
Ubutu wa sheria mbalimbali.
Ukosefu wa vitendea kazi.

ATHARI ZA RUSHWA
Rushwa husababisha madahara mengi katika jamii ambayo huathiri nyanja zote kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na kiasa.
Baadhi ya athari hizo ni:-
Kushuka kwa pato la Taifa.
Kuongezeka gharama zisizo za lazima katika miradi mbalimbali zinazosababisha wananchi kukosa huduma muhimu za kijamii.
Kuvusha nyara za serikali, madini na biashara ya madawa ya kulevya.
Huathiri utekelezaji wa majukumu ya serikali yao mfano kuacha kutoa ushirikiano kwa serikali.
Husababisha wananchi kukosa imani na serikali yao mfano kuacha kutoa ushirikiano kwa serikali.
Hukwamisha utoaji wa haki.
Huogofya wawekezaji.
Huhamisha rasilimali za nchi kwenda kwa wananchi wachache walio na uwezo.
Husababisha kuongezeka kwa maovu katika jamii.
Husababisha kuongezeka kwa maambukizi ya UKIMWI.
Husababisha kuwa na viongozi wasiofaa.
Husababisha vifo.
Husababisha ongezeko la umaskini.
Huathiri misingi ya utawala bora, demokrasia na utawala wa sheria.

WAJIBU WA VIJANA KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA RUSWA
Kila mtanzania anao wajibu wa kupambana na rushwa kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 26, 27 na 28... “Kila mtu ana wajibu wa kufuata na kutii katiba na Sheria za Jamhuri ya Muungano” - Ibara ya 26 (1)...” Watu wote wanatakiwa na sheria kutunza vizuri mali ya mamlaka ya nchi na ya pamoja, kupiga vita aina zote za uharibifu na unadhirifu, na kuendesha uchumi wa Taifa kwa makini kama watu ambao ndio waamuzi wa hali ya baadaye ta taifa lao” -Ibara ya 27 (2). Vilevile Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa kifungu cha 39 kinatamka bayana kwa kila mtu mwenye taarifa kuhusu kufanyika kwa vitendo vya rushwa unaopangwa na mtu au kundi la watu anawajibika kutoa taarifa kwa TAKUKURU. Hivyo katika mapambano dhidi ya rushwa vijana wanapaswa kutekeleza mambo yafuatayo:-

1. Wawe mfano wa kuigwa kwa kutekeleza yafuatayo:-
Kutoshawishi, kutoa au kupokea rushwa ili kupata au kutoa huduma kwa wanajamii au vijana wengine.
Kataa na kukemea rushwa kila inapojitokeza.
Kuwaelimisha wanafunzi, vijana na jamii kwa ujumla juu ya rushwa na hasa madhara yake, haki na wajibu wao kwa njia ya nyimbo, ngonjera, mashairi, maigizo na sanaa mbalimbali. Wanajamii wengine hujihusisha na rushwa kwa kukosa ufahamu.
Kuelimisha jamii faida za kupambana na rushwa kwa kutumia mbinu mbalimbali.
Kujifunza kwa bidii na kuwajibika ipasavyo kwa muda unaostahili kwanii uzembe huzaa vishawishi vya rushwa.
Kutoa ushirikiano wa dhati kwa TAKUKURU na vyombo vingine pindi unapohitajika. Kwa mfano kutoa taarifa kuhusu vitendo vya rushwa vinavyotendeka katika jamii.

2. Wawe jasiri kwa:-
Kukemea vitendo vya rushwa na kuwafichua wale wote wanaoshiriki kufanya vitendo vya rushwa.
Kufichua mianya inayotumiwa na wala rushwa ili iweze kuzibwa.

3. Wawe wazalendo kwa:-
Kufuata sheria, kanuni na taratibu za serikali.
Kutoshawishi, kutoa au kupokea rushwa ili kupata au kutoa huduma kwa wanajamii au vijana wengine.
Kutoa taarifa za ukiukwaji wa maadili kwenye kamati ya maadili ya mtumishi husika.

Chanzo cha habari: Takukuru

VIJANA WA TANZANIA BILA UMASIKINI INAWEZEKANA?

UMASIKINI NI NINI?
Watu tofauti hufasiri maana ya umasikini kwa njia mbalimbali viongozi kwa kawaida hufikiria juu ya umasikini kwa kuangalia uwezo wa watu katika kununua mahitaji yao na kuuza bidhaa zao. Lakini fasiri ya umasikini ni kubwa zaidi. Kuna fasiri ya kuzingatia matatizo ya kuwa na mgawanyo sawa katika kupata elimu na afya bora, kuwa na heshima na hadhi katika jamii, kusikia kuwa na uwezo na kutatua tatizo lolote linalotokea katika maisha yake, na hivyo kuwa na matumaini ya maisha. Kwa hiyo kuna mengi ya kufikiria wakati unapotaka kuondoa umasikini. Kwa hakika fikra nyingi haziko wazi mpaka unapofikiria kwa makini yanayotendeka katika jamii.

Watu wa kawaida, wafanyabiashara, wafanyakazi serikarini, mawaziri na viongozi wa nje wana mawazo tofauti kuhusu swali la umasikini ni nini. Wana mawazo tofauti kuhusu sababu za umasikini na jinsi ya kuondoa.

Wataalamu wanavyolioa suala la Umasikini
Katika dunia ya sasa watu hununua mahitaji yao kwa kutumia pesa. Kama hawana njia za kupata pesa watakuwa maskini. Umasikini mbaya zaidi ni ule ambao unawafanya watu wasiweze kupata chakula. Kwa hali hiyo, wanakuwa dhaifu na wanaweza kufa kwa njaa. Hali nyingine ya umasikini ni ile ambayo watu wanaweza kuwa na chakula kiasi au kidogo lakini hawana maji salama, huduma za matibabu, nyumba au mavazi bora.

AINA YA UMASIKINI
Umasikini wa kipato
Inafikiriwa kuwa wakati mapato ya watu ni chini ya dola moja kwa siku katika nchi zinazoendelea kama Tanzania. Hii ina maana kwamba hawatakuwa na chakula cha kutosha, uwezo wa kupata tiba, watakuwa na mavazi na nyumba duni.

Umasikini usioo wa kipato
Kuna wakati watu wanakuwa na fedha kidogo na hivyo hawawezi kumudu shule nzuri na kuwa na maji salama watu wanaoishi katika umasikini usio na kipato wanategemewa kudumaa na kufa mapema.


Tutapunguzaje umasikini?
Vijana wengi walipoulizwa wajiepushe na nini ili wasiingie katika hali ya umasikini walitoa mawazo yafuatayo:-
Wamiliki ardhi.
Wapate zana za kilimo na technologia..
Waweza kupata masoko kwa urahisi.
Wapate misaada na mikopo.
Kujenga uwezo wa kuweka akiba.
Waweze kupata maji safi na salama.
Wawe na usafiri nzuri (barabara na magari).
Kupunguza rushwa, kuwe na uwazi zaidi, kuimarisha uwajibikaji na ushirikishwaji katika kuchangia kutoa maamuzi katika kiwango cha serikari za mitaa na serikari kuu.
Wapate huduma bora za jamii na miundo misingi (hasa afya na elimu).
Kuunda upya na kuimarisha vyama vya ushirika.
Kuwawezesha wanawake wawe na madaraka zaidi katika kudhibiti mali ya familia.
Kujenga umoja, mshikamano, kuaminiana na hali ya kushirikiana.
Usalama kazini.

Hata hivyo umasikini unaweza kuondilewa kwa kutatua matatizo yafuatayo:-
Kushughulikia tatizo la ajira kwa vijana.
Kuzuia uharibifu wa mazingira.
Serikari kuongeza fedha zilizopo (bajeti) kwa ajili ya kuondoa umasikini.
Kuendeleza mfuko wa fedha ili kusaidia wakulima wadogo wadogo.
Kuwasaidia watu kuendeleza biashara ya kati.
Kuifanya utafiti zaidi ili kugundua jambo gani linapaswa. Kufanywa na tuna uwezo gani wa kulifanya jambo hilo.
Kuzuia ajira kwa watoto.
Kuongeza idadi ya wanafunzi wanajiunga shule za sekondari na vyuo mbalimbali.

Nafasi ya kijana mmoja mmoja katika kupunguza umasikini
Licha ya serikari kuwajibika katika kupunguza umasikini kwa wananchi wake, ipo nafasi ya kijana mmoja mmoja katika kupunguza umasikini:-
Kutafuta uwezo wa kujiajiri.
Kuwa wabunifu katika kazi zao
Kutafuta taarifa na fursa mbalimbali.mf. Soko la Afrika mashariki
Kuungana katika vikundi ili kufanya kazi pamoja.
Kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ili kushiriki katika kufanya uwamuzi wa mambo yanayowahusu.
Kupanga na kutumia muda vizuri.

Kama hayo yote yatafanyika, serikari, wahisani na vijana wenyewe kushiriki katika kutatua swala la umasikini, jibu litakuwa VIJANA WA TANZANIA BILA UMASKINI INAWEZEKANA.

Thursday, September 23, 2010

UMUHIMU NA NAFASI YA VIKUNDI KATIKA MAENDELEO

Vikundi vya maendeleo, ni jukumuiko la wananchi wakeleketwa wenye nia ya kuleta mabadiliko kwa kutumia uwezo na ubunifu wao katika kuamasisha ari ya wananchi kushiriki kwa pamoja katika kutafakari na kutafuta ufumbuzi wa jambo linalohitaji kutafutiwa suluhu. Vikundi vya maendeleo kama ya Elimu, Uchumi, ushawishi na utetezi, kilimo, ufugaji, ujasiriamali, uchangishaji wa fedha, na kutoa huduma mbalimbali kwa jamii. Katika shughuli hizo vikundi vinaweza kuwa kiungo muhimu na imara katika kusonga mbele kwa maendeleo ya wanakikundi wenyewe, jamii na Taifa kwa ujumla wake kwa kutumia vikundi katika maeneo yetu; tunaongeza ubunifu, ufumbuzi wa mambo mbalimbali na kuongeza msukumo katika kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.
Uhuru wa kushirikiana katika katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ibara ya 18 na 20 za katiba ya jamhuri ya Muungano wa Tanzannia zimeweka wazi juu ya haki na uhuru wa mtu binafsi na kikundi kutoa mawazo, maoni au kushirikiana na wengine ili kuleta maendeleo ya jamii na Taifa kwa ujumla.
Yafuatayo yameainishwa wazi kwenye katiba kuhusu haki na wajibu wa jamii na uwepo wa vikundi kwa ajili ya maendeleo:-
Kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni na kueleza fikra zake.
Kila mtu anayo haki ya kutafuta, kupokea na kutoa habari bila kujali mipaka ya nchi.
Kila mtu anao uhuru wa kufanya mawasiliano yake na haki ya kutoingiliwa katika mawasiliano yake.
Kila mtu anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi na pia kuhusu masuala muhimu kwa jamii.
Kila mtu anao uhuru wa kukutana na kushirikiana na wengine kwa ajili ya kutoa mawazo yake hadharani na kuanzia na kujiunga na vikundi, vyama au mashirika yaliyoanzishwa kwa madhumuni ya kuhifadhi, kuendeleza maslahi yake au maslahi mengineyo.
Nguvu na wajibu wa wananchi kuleta mabadiliko kupitia vikundi kwa dhana ya kufanya kazi ya pamoja
Mtu mmoja anapofanya kazi peke yake ni vigumu kubadilisha hali fulani. Anaweza akakosa ujasiri wa kuleta mabadiliko, kuchukua hatua au kutoa maoni na kero zake. Badala yake kikundi cha watu wenye nia madhubuti na imani sawa kuhusu hali fulani wanaweza wakafanya mambo makubwa. Kwa kufanya kazi pamoja na kusaidiana; mabadiliko yanaweza kupatikana tena kwa haraka zaidi. Kufanya kazi pamoja kunasaidia pia kujenga tabia ya kujiamini kama mawakala wa mabadiliko (egents for change ). umoja pia unarahisisha kupata msaada kutoka nje au ndani ya jamii kuliko msaada huo kutolewa kwa mtu au mwanaharakati mmoja.
Kwa ufupi vikundi vina faida zifuatazo:-
Kujenga nguvu na utashi wa pamoja (umoja ni nguvu)
kurahisisha utendaji wa pamoja.
Kubadilishana uzoefu (Kutiana moyo).
Kuelimishana.
Kushirikiana katika matumizi ya rasilimali.
MAKUBALIANO YA KUJIUNGA, KUANZISHA NA KUENDELEZA KIKUNDI
Kuwepo kwa nia ya pamoja.
Kabla ya kuunda kikundi ni lazima kuwepo tatizo/matatizo yanayowaunganisha wanachama wa kikundi na kukubaliana kushirikiana kuyakabili. Wanakikundi wanatakiwa kutambua umuhimu wa kuunganisha nguvu zao kutatua tatizo/matatizo hayo. Pakiwa na haja na nia ni rahisi kwa wanakikundi kukubaliana kwa pamoja kwa kuwa kila mmoja analiona tatizo lililo mbele yake.

Uhiari na utayari wa kujiunga na kikundi
Kimsingi, kujiunga na kikundi ni suala la hiari na kuwa tayari kujitolea kufanya kazi kwa pamoja ili kujiletea maendeleo yao. Kabla ya kujiunga au kuanzisha kikundi ni lazima kila mwanakikundi awe ameamua kwa hiari yake bila kushurutisha au, kushirikizwa maa mtu/taasisi yoyote. Endapo uamuzi wa kuanzisha/kujiunga katika kikundi utakuwa wa kulazimishwa haitakuwa rahisi kwa wanakikundi kukabili majukumu au wajibu kama mwanakikundi.

Tathmini ya aina na msingi wa kikundi
Kikundi kinaweza kuwa chombo kinachojitegemea au kikawa ni sehemu ya kikundi kimoja au taasisi fulani. Uanzishwaji na uendelezwaji wake unategemea sana wanachama wake, hivyo ili kuwa na kikundi chenye sauti na nia moja kuna haja kwa wanachama wake kushiriki kikamilifu katika shughuli za kikundi kwa hiari na kwa kujituma. Siyo vizuri kwa kikundi kuwa tegemezi kwa kiasi kikubwa katika utekelezaji na usimamizi wa shughuli zake.
Msaada toka kwa wadau wengine nje ya kikundi usiwe kipambele bali kichocheo tu katika kuleta mabadiliko. Ili kuleta mwelekeo mzuri wa vikundi hivi, huna haja ya wanakikundi kufanya tathmini yakinifu kutambua aina ya wanachama walionao. Kama kikundi kitakuwa na wanachama wenye moyo wa kujitolea na walio tayari kuleta maendeleo ya kweli basi kikundi hakitaishi kwa utegemezi wa msaada kutoka nje hususani kwa wahisani.

Wanachama mchanganyiko na ushiriki wa makundi maalumu.
Kuwa na kikundi chenye wanachama mchanganyiko wajinsia na makundi mbalimbali ya watu kunatoa fursa ya kujenga kikundi imara chenye uwakilishi sawia. Vikundi vya maendeleo havina budi kuwa na uwakilishi wa makundi mbalimbali ya watu walioko ndani ya jamii kama vile watu wenye ulemavu, wanawake na wajane, maana makundi haya yanahitaji msaada na uprndeleo maalumu katika kushirikishwa katika maamuzi na pia katika maendeleo ya nchi kwa ujumla.
Kujenga mahusiano mazuri
ni vyema kuwa na mahusiano ya karibu (kiutendaji) na watendaji mbalimbali katika ngazi ya kijiji, kata na wilaya. Ni vyema pia kwa kikundi kuzifahamu sera mbalimbali, sheria, kanuni, taratibu na miongozo ya vikundi.
Kujali maslahi ya jamii na nchi
Kikundi kinatakiwa kuwa na mikakati inayochangia na kuchochea maendeleo endelevu ndani ya jamii na nchi kwa ujumla kwa kulingana na sera zilizokubaliwa na wanachama na nchi hali hiyo, kuna umuhimu wa wanachama kuchangia ili kuleta maslahi ya jamii pamoja kulingana na makubaliano ya wanakikundi na wananchi kwa ujumla.

Haja ya kupima utendaji wa kikundi
Kwa kuwa lengo kuu la vikundi ni kutetea na kuchochea maendeleo ya nchini, ni vizuri kikundi kikajenga tabia ya kupima utendaji wake ili kuona ni kwa kiasi gani wamefanikiwa au kutofanikiwa katika kuyafikia malengo na ndoto zao. Kikundi kinapaswa kujua hatima ya jitihada zake ili kuwa na hakika na kile kinachofanywa. Pia kikundi kinaweza kuonisha viashiria walivyojiwekea na vile vilivyowekwa na mipango/mikakati ya serikari na jumuia ya kimataifa.
Vikundi ni mojawapo ya mihimili itakayokuwa na nguvu kuleta maendeleo katika jamii husika. Vikundi havina budi kujipanga vyema ili kuweza kuhimili mikiki mikiki ya harakati za maendeleo ya jamii.
Pia, vikundi havina budi kufuata taratibu na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuepuka kuwa na mitazamo ya kidini, ushabiki wa kisiasa, Ukabila, ubaguzi wa aina yoyote ile na vitendo vya kihuni.

KIJANA WA KISASA NA KILIMO KWANZA

Kuajiriwa na kujiajiri ni changamoto kubwa zinazomkabili kijana ambaye yuko shuleni/chuoni na anatarajia kumaliza masomo yake baada ya muda mfupi. Vijana wengi wamekuwa wakifikiri waajiriwe wapi na kwa mshahara kiasi gani, katika biashara gani ambayo itawaingizia kipato cha kujikimu.
Kilimo ni moja ya shughuli rasmi ambayo kijana anaweza kujiajiri na kupata kipato. Ila ni vijana wachache ambao wamewahi kufikiri kuwa kilimo kinaweza kuwakomboa katika umaskini wa kipato. Kilimo kimedhaniwa kuwa ni shughuli inayofanywa na watu wanaoishi vijijini ambao hawajasoma na wamekosa uwelekeo katika maisha. Ndio maana mtu akiyumba katika maisha awapo mjini au akifeli shule watu humshauri aende kijijini akalime. Shughuli za kilimo zimechukuliwa kuwa ni shughuli ambayo haihitaji utaalamu. Mashuleni, mitaani na Vyouni, vijana wengi wamekuwa wakikebehi kilimo bila kujua bila kilimo wasingekuwa hapo walipo. Vijana wengi wanafikiri kufanya kazi za ofisini na wengine wanafirikiri kujiajiri katika biashara za kukaa dukani na kusubiri wateja.
Umuhimu wa kilimo unaonekana wazi kabisa kwani asilimia 80 ya watanzania wanategemea kilimo, huku kilimo kikichangia asilimia 26.7 ya pato la Taifa. Kilimo kinachangia asilimia 95 ya chakula kinachotumika nchini, asilimia 30 ya mauzo nje na asilimia 65 ya malighafi zinazotumika katika viwanda vyetu vya ndani Tanzania imejaaliwa kuwa na hekta milioni 44 za ardhi inayofaa kwa kilimo lakini ni asilimia 23 tu ndio inayotumika. Kuna hekta milioni 29 zinazofaa kwa kilimo cha umwangialiaji na maji ya kutosha yapo lakini ni asilimia 1 tu iliyo chini ya umwangialiaji. Je, hizo sio fursa kwa kijana wanaotaka kujiajiri kupitia kilimo?
Wapo vijana ambao wanajishughulisha na shughuli za kilimo, vijana hawa wamefanya shughuli hizi kwani ni mbadala baada kukosa shughuli nyingine za kufanya. Vijana hawa wamekuwa wakikabiliwa na changamoto nyingi mojawapo ya changamoto hizi ni:-

  • Ukosefu wa mtaji kulima kilimo cha kibiashara.

  • Ukosefu wa zana bora za kilimo mfano:- Matreta.

  • Wadudu waaribifu wanashambulia mazao.

  • Kilimo cha kutegemea mvua.

  • Ukosefu wa taarifa mbalimbali za kilimo na fursa zilizopo.

  • Ulanguzi wa bei sokoni baada ya kufa kwa vyama vya ushirika.
Kutokana na changamoto hizo ziko changamoto ambazo ziko ndani ya uwezo wa kijana wakisasa na zipo changamoto nyingi ambazo haziko ndani ya uwezo wa kijana.
Matatizo haya yanaweza kutatuliwa kwa:-

  • Kwanza, vijana waone kuwa shughuli za kilimo ni rasmi na kijana yeyote anaweza kujiajiri kupitia shughuli za kilimo.

  • Vijana wafahamu fursa mbalimbali zinazotokana na kilimo.

  • Serikari ichukue nafasi yake kwa kutimiza nguzo kumi za KILIMO KWANZA ambazo wamezitambulisha, nguzo hizo ni:-

  1. Utashi wa kisiasa kutoa msukumo wa mapinduzi ya kilimo

  2. Kugharamia mapinduzi ya kilimo.

  3. Uboreshaji wa mfumo wa utawala wa kilimo.

  4. Mabadaliko ya mfumo wa mkakati katika kilimo.

  5. Upatikanaji wa ardhi kwa ajili ya kilimo.

  6. Vivutio vya kuchochea uwekezaji katika kilimo.

  7. Uendeshaji wa viwanda katika kuleta mapinduzi ya kilimo.

  8. Sayansi, Technologia na Rasirimali watu katika kuwezesha mapinduzi ya kilimo.

  9. Uendesha wa miundo mbinu ili kuwezesha mapinduzi ya kilimo.

  10. Uhamasishaji na ushirikishwaji wa watanzania kuunga mkono na kutekeleza KILIMO KWANZA.
Kutokana na umuhimu huo wa kilimo vijana wa kisasa hawapaswi kupuuza shughuli za kilimo kwamba haziwafahi. Kilimo ni muhimu sana katika maendeleo ya nchi yetu kwani hutupatia chakula, ajira na hukuza pato nchini kwa ujumla.
Na. Innocent. J. Mbele
Mwenyekiti, FASO.

Friday, September 17, 2010

MAKALA NDANI YA BLOGU

Sasa tunakuletea makala mbalimbali katika blogu hii.Makala zitahusu vijana,uchumi,siasa,michezo,kilimo na biashala.KAA TAYARI.

MAJINA YA WANAKIKUNDI NA NAMBA ZA VIKUNDI VYAO WALIOJIUNGA NA FASO KATIKA KATA YA KAHE KIJIJI CHA NGASINYI-2010

FG-A01
1.       Steven Jeremia
2.       Samson Simson
3.       Stanley Philipo
4.       Prisca John
FG-A02
1.       SantielSauli
2.       Mary Daniel
3.       Magdalena Malisa
4.       Julius Mwandandila
FG-A03
1.       Estomin N Mlay
2.       Sharifa S Mdee
3.       Nelson J Kimati
4.       Nipaeli Japhet Mmanyi
FG-A08
1.       Delfina Meshaki
2.       Benjamin Rajabu
3.       Bedasto Fidelisi
4.       Agnes Joshua
FG-A07
1.       Daniel R Kimati
2.       Nganasho A kasote
3.       Faustin s Masawe
4.       Mery F Massawe
FG-A06
1.       Marystela Paul
2.       Living’s Fataely
3.       Kundaely Charles
4.       Jeremia AJefta


FG-A05
1.       Semu John
2.       Santiel Jacob Kimati
3.       Elisante I Mmanga
4.       Agnes J Mmanga
FG-A04
1.       Willium A Kimati
2.       Elybrown Ralph
3.       Haines M Mmanga
4.       Rose A Mtey                            

MASHARTI YA UTUNZAJI WA FEDHA NA MALI ZA KIKUNDI-2010


YALIYOMO
                                                                                                     _________________

                                                                                                                         Ukurasa                                                                                                                          
1. UTANGULIZI----------------------------------------------------------------------------

2. FEDHA ZA KIKUNDI------------------------------------------------------------------

3. UTARATIBU WA KUREKODI NA KUTUNZA MAPATO-------------------

4. UTARATIBU WA KUFANYA MALIPO--------------------------------------------

5. KUPOKEA NA KUHIFADHI MAZAO----------------------------------------------

6. UTARATIBU WA HIFADHI YA BIDHAA/VIFAA-------------------------------

7. UPOKEAJI NA UTUNZAJI WA HISA BIDHAA /DUKANI--------------------

8. MALI ZA KUDUMU---------------------------------------------------------------------

9. UWEKAJI WA HISA ZA WANAKIKUNDI---------------------------------------

10. MGAO WA ZIADA---------------------------------------------------------------------

11. UKODISHAJI WA PEMBEJEO KWA WANAKIKUNDI--------------------

12. SALIO BAADA YA UZALISHAJI-------------------------------------------------

1. UTANGULIZI

Kikundi cha FASO ni chombo kamili cha kuzalisha mali.Ili chombo hiki kiweze kufanikiwa ni budi kuwe na utaratibu mzuri wa utunzaji wa fedha/vifaa pamoja na matumizi yake; na hili hufanyika kwa kuweka kumbukumbu kadha.Baadhi yake zikiwa ni hizi zifuatazo ambazo lazima kikundi kiwe nazo:-
1. Stakabadhi ya fedha (cash receipt vouchers)
2. Hati ya malipo (Payment voucher)
3. Daftari la fedha (Cash Book)
4. Hati za kupokelea na kutolea vifaa/bidhaa (Receipt Issue vouchers/stores)
5. Kadi ya mazao na mali (Stock cards)
6. Leja (Ledgers)
7. Jono (Journal-yaani hati za makopesho au masawazisho)
8. Daftari la Wanakikundi (Membership register)
9. Stakabadhi ya mafungu (Share receipt book)
10. Hati ya mali (stock certificate)
11. Hati ya fedha mkononi (Cash balance certificate)
12. Daftari la orodha za mali ya kudumu (Inventory of Assets)
13. Daftari la fedha mkononi kila siku (Daily Cash Balance)
14. Jalada la hati ya udhibitisho wa uuzaji wa mazao (Credit note from various crops authorities)
15. Hati daiwa/Akra za madai (Debit Note/Invoice)
16. Hati ya kusafirisha mazao (Consignment notes)
17. Hati ya ununuzi mafungu (Investment Certificate)
18. Vitabu vya stakabadhi ya mazao (Produce receipt Book)
19. Kitabu cha kumbukumbu ya mikutano (Minutes Book)
20. Urari wa kila Mwezi (Monthly Trial balance)
21.Orodha ya wadaiwa (List of Debtors)
22. Orodha ya wadaiwa (List of Creditors)
23. Hesabu za Mapato na Matumizi (Income and Expenditure Account)
24. Waraka wa Mizania (Balance Sheet)
25. Makadilio ya mapato na matumizi (Estimated income and Expenditure)
26. Taarifa za Benki za kila mwaka (Bank Statement and Pay-in-Slip)

2. FEDHA ZA KIKUNDI
-Fedha za kikundi zitatokana na :-
A) Kiingilio (1,000/=), ada ya uwanakikundi (2,000) na michango maalumu B)Ruzuku na misaada C) Hisa za wanakikundi D) Ziada halisi E) Mikopo toka mabenki na taasisi nyingine za kifedha

3. UTARATIBU WA KUREKODI NA KUTUNZA MAPATO:

a)      Fedha za aina yoyote ile zinazoingia katika Kikundi kwa njia ya hundi, fedha taslimu, n.k ni lazima stakabadhi ya fedha itolewe kudhibitisha kuwa Kikundi kimepokea fedha hizo. Stakabadhi ya fedha hizo lazima itolewe wakati huo huo fedha inapopokelewa na nakala halisi ya stakabadhi sharti apewe mtu aliyewasilisha hizo fedha.
b)      Hairuhusiwi kufutafuta, kubadilisha au kukata ovyo stakabadhi iliyoandikwa; endapo kuna makosa katika uandikishaji wa stakabadhi, basi lazma Mwenyekiti/katibu aarifiwe ndipo stakabadhi hiyo ifutwe (Cancel), na hiyo iliyokosewa lazima ibakie kwenye kitabu cha stakabadhi.
c)      Kila stakabadhi lazima itiwe sahii na Mhasibu wa kikundi/mpokeaji
d)     Vitabu vya stakabadhi vilivyotumika na vile ambavyo havijatumika vitunzwe vizuri ili viweze kukaguliwa na wakaguzi.
e)      Fedha zote ambazo zimepokelewa kwa mfano fedha za kukodisha pembejeo, mauzo ya bidhaa za duka, na mapato mengineyo, iingizwe katika daftari ya fedha (Cash Book) siku hiyo hiyo.
f)       Mahali palipo na tawi la Benki itabidi pia fedha zote zilizopokelewa zipelekwe Benki chini ya ulinzi madhubuti kila siku. Hii ina maana kwamba fedha zinazopelekwa baada ya saa hizo ni budi zihifadhiwe kwenye sefu ya kikundi hadi kesho yake na liwe ni jukumu la kwanza kuzipeleka fedha hizo Benki kesho yake.Fedha zote lazima zihifadhiwe kwenye Sefu imara ya Kikundi; atakaye kiuka atachukuliwa hatua za Kisheria/kinidhamu.  
g)      Sefu budi iwe imara ijengwe ukutani kwa kutumia saruji au chuma ngumu pia iwe na kufuri mbili zilizo tofauti. Funguo za sefu lazima zitunzwe na watu wawili kama fuatavyo:-
                                    1. Mhasibu wa Kikundi (Mtunza hazina wa kikundi)
                                     2. Mwenyekiti wa Kikundi  
h)      Kwa kawaida sefu huwa na nakala mbili za funguo (original and duplicate keys). Hivyo funguo mbadala ni lazima zikabidhiwe kwa Katibu wa kikundi kwa ajili ya kuhifadhiwa na itabidi hati maalumu itolewe na kusainiwa ili kuthibitisha kuwa wamepokea kifurushi kilichofungwa (sealed) chenye funguo hizo.
i)        Uandikaji wa kitabu chakutunzia fedha (cash book) iwe ni kazi ya kila siku na itabidi baki (balance)  iliyoko baada ya kuondoa matumizi ionyeshwe na iwe imethibitishwa na Mhasibu wa kikundi pamoja na Katibu.
j)        Kwa kawaida kikundi kitakuwa kinatunza daftari za fedha (cash book) mara mbili ama tatu kulingana na shughuli zake, mfano mapokezi ya fedha za ununuzi wa mazao (Produce cash book) na yale ya ,Ruzuku,Ada, n,k.yaingizwe katika daftari la kawaida (General Cash Book) Ni marufuku kuingiza fedha za mazao katika daftari ya kawaida ama fedha za hisa katika daftari ya mazao ;na ikiwa maingizo hayo yamefanyika kwa makosa ni budi kufanya masahihisho kabla ya kufunga kazi za siku ile.
k)      Baada ya shughuli za kila siku ni budi upungufu wowote utakaoonekana katika daftari ya fedha uarifiwe kwa kamati ya ukaguzi/katibu wa kikundi na hatua za kisheria/kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya wanaohusika bila kuchelewa.
l)        Mahesabu yote baada ya kuingizwa kwenye daftari ya fedha (Cash Book) ni lazima pia yaingizwe kwenye leja kufuatana na hesabu (accouts) mbalimbali zilizowekwa. Maingizo kwenye leja yawe yakifanyika kila mara hasa kila wiki (hasa jumamosi)  kuingiza muktasari wa mapato hayo kwenye leja.

4. UTARATIBU WA KUFANYA MALIPO:
a)      Ni lazima malipo yote yaandikiwe Hati za malipo ambazo ni budi ziidhinishwe na Mwenyekiti/katibu wa kikukudi kabla Mhasibu wa kikundi hajafanya malipo yenyewe.Ni marufuku kabisa kufanya malipo ambayo hayajakubaliwa na ambayo hayako katika makisio yaliyoidhinishwa.
b)      Malipo yote yatafanywa kwa hundi isipokuwa matumizi madogo madogo yasiyozidi 100,000/=.
c)      Hati ya malipo ni lazima zitiwe sahihi na mlipwaji au Hati ya madai pamoja na stakabadhi ya kuthibitisha kwamba mlipwaji amepokea hayo malipo, iambatanishwe na hati ya malipo. Kutokufanya hivi malipo hayo yatatiliwa mashaka na anayehusika atachukuliwa hatua za kisheria.
d)     Ikiwa malipo yamefanyika kwa ajili ya kulipa deni ambalo ankra yake imekwishapolewa ni budi hiyo ipigwe mhuri wa kuonyesha kwamba malipo yasije yakafanyika mara mbili.

5. KUPOKEA NA UTARATIBU WA KUIFADHI MAZAO          
a)      Mazao yateuliwe (Grades) na kupimwa na Katibu na kukaguliwa na kamati ya ukaguzi.
b)      Mazao lazima yahifadhiwe katika ghala/stoo ambayo ni imara.
c)      Mazao yote yanayonunuliwa/kuingia kwenye ghala/stoo.
d)     Mazao yanayotolewa ghalani lazima mtunza ghala/stoo atoe hati ya kutolea mazao (Godown issue voucher)
e)      Hati za kupokelea na kutolea mazao lazima ziingizwe katika kitabu cha mazao ghalani/stoo (Goodown Produce Stock Book) au kwenye kadi mazao ghalani (Produce Card).
f)       Kama kutatokea upungufu usio wa kawaida lazima hatua za kisheria zichukuliwe.

6. UTARATIBU WA HIFADHI YA BIDHAA/VIFAA       
Bidhaa zote kama mbolea, majembe, mbegu, na bidhaa zingine ambazo zinahusiana na shughuli za uzalishaji mali kikundini (Farm inputs etc) lazima zihifadhiwe kwenye stoo imara na utaratibu wake utakuwa kama kwenye hifadhi ya mazao (Na.4 (b)-(g)  

7. UPOKEAJI NA UTUNZAJI WA BIDHAA DUKANI 
Utaratibu kama ulivyoelezwa katika Aya ya 4- kuhusu hifadhi ya mazao utafuatana na kuzingatiwa kwa dhati.
Kwa kifupi utaratibu wa utunzaji wa mazao, vifaa na bidhaa za duka ni mmoja, na bodi ya uongozi lazima wahakikishe kwamba mali hizi zinatunzwa na kulindwa ili zisitumike vibaya na wanaohusika.

8. MALI YA KUDUMU:
a)      Ununuzi;
Kikundi kitafanya ununuzi wa mali ya kudumu kulingana na mahitaji ya kikundi.Bodi ya uongozi itapendekeza na kupitisha manunuzi ya mali zote za kudumu.

b)     Utunzaji
Kikundi kitatunza daftari ya orodha za mali ya kudumu (Register of Inventory of Assets) ambamo kila mali ya kikundi itaingizwa.Endapo kikundi kitauza mali yoyote ile itarekodiwa katika kitabu hiki.

c)      Uuzaji
Iwapo kikundi kitauza mali ya kudumu, kitafanya hivyo kwa kutumia njia ya zabuni ambazo Kamati ya fedha na Mipango itatoa uamuzi wa mnunuzi wa mali hiyo.

9. UWEKAJI WA HISA ZA WANAKIKINDI
a.       Hisa ni sehemu ya mtaji wa kikundi ambao mwanakikundi anachangia kudumisha mtaji wa kikundi na sehemu ya hakiba ya mwanakikundi katika kikundi.Mwisho wa mwaka wa fedha faida itagaiwa kwa mwanahisa kulingana na idadi ya hisa walizonazo.
b.      Thamani ya hisa moja itakuwa ni shs 3000/= na kila mwankikundi anatakiwa kuwa na angalau hisa mbili au zaidi ndani ya mwaka mmoja.
c.       Mwanakikundi atakayetaka kuchukua hisa zake zote atoe taarifa kwa maandishi na atarudishiwa hisa zake baada ya siku 60.
d.      Hisa ni akiba ya mwanakikundi katika kikundi.
e.       Faida itagawiwa kila mwaka kulingana na faida za uzalishaji zilizotokana na uzalishaji wa hisa hizo.
f.       Fedha za hisa za wanakikundi zitatumika katika uzalishaji mbalimbali ulioidhinishwa na bodi au kuongeza mtaji wa kikundi.
g.      Mwanakikundi mmoja hataruhusiwa kuwa na hisa zaidi ya 2/5 ya hisa zote kikundini.
h.      Mwanahisa ataruhusiwa kuchukua faida kutoka katika hisa zake mara baada ya faida ya hisa kutangazwa kama atapenda kufanya hivyo.Vilevile faida ya hisa inaweza kubaki kikundini ili kuongeza hisa za mwanachama.
i.        Kila mwanakikundi atamteua mrithi wake ambaye atakuwa na haki ya kurudishiwa hisa au faida zitakazopatikana kila mwaka.
10. MGAO WA FAIDA
a) Kila msimu kikundi kitatenga Asilimia 12% kutokana na faida halisi kwa ajili ya mfuko wa ukuzaji wa mtaji (Capital Development Fund)
b) Kila msimu kikundi kitatenga Asilimia mbili (1%) kutokana na faida halisi kwa ajili mfuko wa maendeleo ya jamii (Social Development Fund)
c) Vile vile kikundi kitatenga Asilimia mbili (2%) kutoka katika faida halisi ya kikundi kwa ajili ya mfuko wa bima ya kikundi. d) Kikundi pia kitatenga Asilimia moja (2%) ya faida halisi ya kikundi kwa ajili ya mfuko wa Elimu ya Kilimo kwa wanakikundi. (kama; gharama za mkutano, semina, mafunzo n.k)

11. UKODISHAJI WA PEMBEJEO KWA WANAKIKUNDI
a) Kikundi kitakodisha pembejeo kwa wanakikundi kulingana na mchanganuo wa mahitaji ya Kilimo husika.
b) Kikundi hakitakopesha fedha isipokuwa kama kuna ulazima wa kufanya hivyo.
c) Bodi ya uongozi Ndiyo yenye mamlaka ya kupitisha thamani ya mkopo/pembejeo zilizoombwa na vikundi.
d) Kamati ya ukaguzi ndio yenye mamlaka ya kukagua na kupitisha Taarifa ya makadilio ya pembejeo zilizopendekezwa na kikundi na kupeleka Taarifa hizo kwa bodi ya uongozi.
e) Mazao yote yatauzwa na kikundi cha FASO kwa bei ilinayokubalika na kutoa ghalama zote pamoja na michango,faida inayobaki itagaiwa kwa wanakikundi.
h) Wanakikundi husika waliokabidhiwa pembejeo watakuwa na wajibu wa kutunza mali hizo. Hatua za kisheria zitachukuliwa kwa upotevu wa mali za kikundi kizembe.
i) Hati maalumu ya kukabidhi pembejeo itajazwa na wanakikundi wote wa kikundi husika na kusaiwa na viongozi wa FASO.

12. SALIO LA ZIADA.
- Salio la fedha litakalobaki baada ya uzalishaji/matumizi ya mradi, fedha hizo zinaweza:-
a) Kuhifadhiwa benki kwa akaunti ya mda mrefu (fixed account) ili kuleta faida
b) Kukopesha fedha hizo kwa wanakikundi kwa makubaliano ya riba nafuu.


xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Monday, September 13, 2010

UFAFANUZI

“KILIMO KWA CHAKULA AJIRA NA MAENDELEO,KWA PAMOJA TUNAWEAZA"


Jina la kikundi: FUMBUKA Agro Solution Group.

Jina la Ufupisho: FASO Group

Jina la mwanzilishi: Innocent John Mbele.

Makao Makuu ya kikundi -kata ya KAHE, kijiji cha Ngasini.

Eneo la shughuli za kikundi -Moshi Vijijini.



Utangulizi;

FASO ni kikundi kilichoanzishwa kwa lengo la kuwaunganisha wakulima wadogo (hususani vijana) ili waweze kujihusisha na kilimo cha uwakika kwa pamoja. Kikundi hichi kilianzishwa na ndugu Innocent J Mbele akishilikiana na vijana wenzake ambao ni Fredrick Mahinya. Mchakato wa kuanzisha kikundi hichi ulianza mwezi februari,2010.Kikundi kilisajiliwa rasmi 30/04/2010 na Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya moshi vijijini na kupewa na


NIA NA MADHUMNI YA KIKUNDI.

a) Kuunga mkono mapinduzi ya kilimo kupitia sera ya Serikari ya “kilimo kwanza”, kwa kuwahamasisha vijana wajihusishe na shughuli za kilimo.

b) Kuwaunganisha vijana katika vikundi vidogo ili waweze kujihusisha na kilimo cha pamoja.

c) Kukodisha pembejeo za kilimo na mashamba kwa wanakikundi kwa masharti nafuu.

d) Kutafuta Soko la uwakika la mazao yanayolimwa na wanakikundi na jamii ya wakulima inayowazunguka.

e) Kuhimiza kilimo cha uwakika kisicho tegemea mvua (kilimo cha umwagiliaji)

f) Kuwaunganisha wanakikundi na wataalamu mbalimbali wa kilimo ili kupata elimu ya kilimo cha kisasa pamoja na elimu ya ujasilia mali.

g) Kuhifadhi na kusindika mazao yalimwayo na wakulima.

h) Kutoa mchango wa maendeleo ya jamii mfano kuchangia chakula mashuleni upandaji wa miti pembezoni mwa vyanzo vya maji, utoaji wa elimu ya Ukimwi kwa jamii husika n.k .


Mikakati

“Kuongeza upatikanaji wa chakula, ajira na Maendeleo kwa vijana na jamii inayowazunguka kwa ujumla”

Mipango

“Kuondoa umaskini kwa kuboresha kilimo kupitia usambazaji wa pembejeo na utoaji wa taarifa za kilimo pamoja na masoko kwa wakulima wadogo”

Dira

Maono ya kikundi ni “kuwa taasisi/ shirika lisilo la kiserikali ambalo litashawishi Maendeleo ya kilimo Tanzania kwa kutoa taarifa mbalimbali za kilimo, kusambaza pembejeo na kutoa huduma za kijamii kwa wakulima ”

Kauli mbiu

“Kilimo kwa chakula, ajira na Maendeleo kwa pamoja tunaweza”

SIFA ZA MWANAKIKUNDI

-Awe kijana mwenye umri kati ya miaka18-35

-Awe mwenyeji wa eneo la mradi.

-Awe mwaminifu/asiwe mwizi na mwongo.

-Awe na akili timamu.

-Awe anapenda ushirikiano.

-Awe mchapakazi.

-Asiwe mlevi kupita kiasi.

-Awe mtanzania.

-Asiwe mbaguzi wa rangi, kabila, ukoo au jinsia.

-Atambulike na uongozi wa mtaa /kijiji/ kata.

Majukumu (wajibu) wa Mwanakikundi

-Kushirikiana na wenzake kufanya kazi za kikundi

-Kulinda mali za kikundi .

-Kutoa michango mbalimbali itakayotolewa na kikundi.

-Kushiriki katika kazi za kijamii.

-Kubeba dhamana ikiwa janga lolote litatokea.

-Kulipa gharama za upotevu wa makusudi wa mali za kikundi

Haki za Wanakikundi

i) Kushiriki katika shughuli zote za kikundi hiki kwa kufuata sheria na taratibu zilizowekwa.

ii) Kutoa maoni yake katika mikutano ya kikundi hiki.

iii) Kuchaguliwa kuwa mjumbe /kiongozi na kuchagua wajumbe /viongozi wa chama hiki.

iv) Kupitia masharti, mizania, muktasari ya mkutano mkuu na nyaraka zote na taarifa za mwezi na mwaka za kifedha.

v) Kununua hisa za kikundi kwa idadi isiyozidi (2/5) 40% ya hisa zote za kikundi.

7.4 Kusimamishwa au kuachishwa Uanakikundi.

-Kushindwa kushiriki katika kazi za kikundi bila taarifa / sababu yeyote.

-Kufanya kitendo chochote ambacho bodi itaridhia kuwa ni cha kutokuwa mwaminifu ambacho ni kinyume na madhumuni ya uanachama

-Kushindwa kufikia kiwango cha hisa kilichoweka kwa mwaka.

-Kukisababishia kikundi hasara kwa uzembe wa makusudi.

-Kutoudhuria mkutano mkuu wa kikundi mara tatu mfululizo bila sababu ya msingi.

7.5 Uwanakikundi Utakoma kwa :-

a) Kujiuzulu mwenyewe baada ya kutoa taarifa kwa maandishi kwa bodi ya Uongozi.

b) Kifo.

c) Kuchukua hisa zake zote kikundini.

d) Wazimu uliothibitishwa.

e) Akiama eneo husika.

f) Kukataliwa uanachama na theruthi mbili (2/3) ya wanachama walioudhuria mkutano mkuu baada ya kupewa nafasi ya kujitetea baada ya kutenda makosa ambayo yanalazimu kukataliwa uwanakikundi

g) Kufilisika kwa Kikundi.

h) Mtu aliyeacha au kufukuzwa uwanakikundi anaweza kujiunga tena kwa mujibu wa masharti haya. Hata hivyo mwanakikundi aliyewahi kujiuzulu/kufukuzwa itabidi apate idhini ya mkutano mkuu ya kujiunga tena na kikundi.

Vikundi Vidogo Vidogo

- Vitakuwa na wanakikundi 3.-6.

-Kila kikundi kitaandaa mchangano wa kilimo/ufugaji wanaotaka kuufanya na gharama zake.

-Kikundi kitashirikiana na kufikisha taarifa za utendaji mara kwa mara kwa katibu wa kikundi.

-Kila kikundi kitapanga eneo la uendeshaji wa kilimo/ufugaji na kukaguliwa na kupitishwa/ kukataliwa na bodi ya uongozi.

-Kila kikundi lazima kiwe na msichana angalau mmoja au zaidi

-Kila kikundi kitamchagua msimamizi /mwakilishi wake mmoja.

FEDHA ZA KIKUNDI.

-Fedha za kikundi zitatokana na

. A) Kiingilio,ada na michango maalumu. B) Ruzuku na misaada C) Hisa za wanakikundi D) Ziada halisi. E) Mikopo kutoka mabenki na taasisi nyingine

-Kiingilio katika kikundi ni Tshs 1000/= kwa kila kikundi.

-Ada ya uwanakikundi ni Tshs 3000/= kwa mwaka.

-Kila mwanakikundi anaruhusiwa kuwa na hisa katika kikundi.Kila hisa moja ina thamani ya Tsh 3000/=

-Kila msimu kikundi kitatenga asilimia 12% kutokana na faida halisi kwa ajili ya mfuko wa ukuzaji wa mtaji.

-2% kutoka katika faida halisi kwa ajili ya mfuko maendeleo ya jamii (Social development fund)

-2% katika faida halisi kwa ajili ya mfuko wa bima ya kikundi.

-1% ya faida halisi ya kikundi/vikundi vidogo vidogo kwa ajili ya mfuko wa Elimu ya kilimo.

Anwani

Kahe-Moshi, Tanzania

Simu: 0715 571 301 or

0765 571 301

Barua Pepe: faso.group@yahoo.com