Friday, June 27, 2014

WAKULIMA WAFUNDISHWA JINSI YA KUANDAA UDONGO WA KITALU

Shirika la FASO likishirikiana na mtaalamu wa kilimo kutoka shirika la TAHA wametoa elimu kwa wakulima wa kijiji cha Ngasinyi, Moshi vijijini. Katika elimu hiyo Afisa kilimo kutoka shirika la TAHA, ndugu Gilliard alitoa elimu ya kuandaa udongo kwa kuuchoma udongo ili kupunguza wadudu.  Elimu hiyo itawawezesha wakulima kutotumia dawa za kemikali katika kukabiliana na wadudu. Hatua hiyo ni mwanzo wa shamba darasa la nyanya litakalo andaliwa kwapamoja.

Wakulima wakiandaa udongo kwa ajili ya kitalu.


Udongo ukichemshwa ili kuua wadudu.

Wakulima wakishuhudia udongo unavyochomwa

Afisa kilimo kutoka TAHA, Ndg Gilliard akikoroga udongo


Udongo ukipakuliwa teyari kwa kuanza kutumika

Afisa kilimo akiupooza udongo uliochomwa.

No comments:

Post a Comment