Thursday, May 9, 2013

Ufugaji wa nyuki ni kazi nzuri ya ziada

Ufugaji wa nyuki unaweza kuwa chanzo kizuri cha kipato cha ziada kwa wakulima wadogo wadogo.

Uzalishaji wa asali nchini Tanzania umekuwa ukitegemea sana wafugaji wadogo wadogo, wanaotumia njia za kiasili kama vile mizinga ya magogo au vyungu, kwa nyuki wa kiafrika ambao ni wengi sana kwenye mapori.


Ni muhimu kuwa na utaalamu wa kufuga nyuki


Mkulima ambae anahitaji kufuga nyuki ni lazima awe na uelewa wa mzunguko wa maisha ya nyuki. Anaye anza ni lazima aulize wafugaji wenzake ambao wana uzoefu wa kutosha, au kujiunga katika kikundi cha ufugaji ili apate ufahamu zaidi juu ya ufugaji wa nyuki.


Tafuta sehemu salama kwa ajili ya mzinga


Ni vizuri kutafuta mahali pazuri, salama, na penye sifa ya kufugia nyuki. Vifaa vyote vikishapatikana jambo linalofuata ni kuchagua mahali gani pa kuweka mzinga. Ni vizuri sehemu hii ikawa mahali ambapo makundi ya nyuki hukusanyika mara kwa mara.


Ni wapi pa kuweka mzinga!


Mara nyingine kupata eneo sahihi ni tatizo. Ni vizuri kuzingatia yafuatayo:


• Kulingana na hali ya kujilinda ya nyuki wa Afrika, haishauriwi kuweka mzinga shambani au karibu na shamba (weka umbali wa mita 150-200 kutoka kwenye mazao au nyumbani)
• Mzinga ni lazima uwekwe sehemu ambayo haitasababisha upotevu wa nyuki wanaporudi kutoka nje ya mzinga (wasiingie kwenye kundi lisilokuwa lao)
• Mizinga isiwekwe mbalimbali sana ili kuepusha usumbufu wa kutembea mbali kwa mfugaji wakati anapokagua. Eneo la kuweka mizinga ni lazima liwe :
• Kimya na mbali ya jumuia (hospitali, shule, na viwanja vya michezo) na maeneo ya biashara au viwanda.
• Karibu na maji masafi-kandokando ya mto, mabwawa ya samaki, mabeseni ya maji au sehemu ya matone.
• Iwe karibu na chakula cha nyukimimea inayochanua, miparachichi,
nazi, euculptus, migunga n.k
• Iwe sehemu ambayo ni kavu na isiwe sehemu ya tindiga kwani unyevu unyevu husababisha ugonjwa wa ukungu (fungal disease) na pia huzuia utengenezaji mzuri wa asali.
• Iwe mbali na watu waharibifu na iliyojificha kuepuka waharibifu.
• Sehemu ya mizinga ni lazima iwe inafikika kirahisi kwa kipindi chote cha mwaka ili iwe rahisi kuhamisha nyuki pale inapohitajika.
• Kuwe na kivuli cha kutosha hasa wakati wa mchana jua linapokuwa kali, na kusiwe na upepo mkali.
• Iwe mbali na mashamba, ambapo dawa za kuulia wadudu zinatumika.
Vichaka au wigo unaotenganisha mizinga na kuzuia wavamizi ni muhimu ili kupunguza ukali wa nyuki.


Jinsi ya kuweka mzinga


Baada ya sehemu ya kuweka mizinga kupatikana, kinachofuata ni kuandaa mizinga kwa ajili ya kuweka panapotakiwa.
• Safisha mzinga kuondoa uchafu wote, utando wa buibui na aina nyingine za wadudu.
• Weka chambo kwenye mzinga (waf ugaji wa nyuki mara nyingi hutumia nta) kwa kuipaka katika kuta za mzinga kwa ndani.
• Mzi nga unaweza kutundikwa kwenye mti, kwenye nguzo, kuweka kwenye jukwaa au kwenye miamba. Hii inategemea mkulima mwenyewe anapendelea njia ipi.


Aina za mizinga ya nyuki


Kifuniko juu (Top bar)


Hii ni aina ya mizinga inayotumika sana. Gharama yake ni karibi shilingi elfu hamsini za kitanzania. Ni aina nzuri sana kwa mtu anaeanza ufugaji wa nyuki kwa kuwa ni wa gharama nafuu. Hata hivyo mfugaji wa nyuki anaweza kutengeneza mzinga mwenyewe kama ana utaalamu wa useremala.


Faida


• Ni rahisi kukagua asali iliyo tayari.
• Ni rahisi kuvuna asali kuliko kuvuna toka kwenye mzinga wa kienyeji.
• Ni rahisi kuwatunza nyuki wakati wa kiangazi na inapokuwa hakuna maua. Mfugaji anaweza kuwapatia nyuki chakula ili kuongeza uzalishaji wa asali.
• Kurina asali ni rahisi sana ukilinganisha na mizinga ya magogo inayotundikwa juu ya mti, kwa kuwa haihitaji vifaa maalumu.
• Aina hii ya mizinga huwekwa kwa kuninginia jambo ambalo siyo rahisi kushambuliwa na wadudu/wanyama wanaokula asali. Inajaa haraka sana wakati ambao ni msimu wa asali kutengenezwa kwa wingi.


Hasara


• Kichane kwenye mzinga wa boksi hakina kishikizo hivyo huvunjika kwa urahisi sana kama hakitashikwa kwa uangalifu.
• Masega huvunwa pamoja na asali, jambo linalolazimu nyuki kutengeneza tena masega mengine na husababisha kupungua kwa uzalishaji wa asali.


Mzinga wa Langstroth unaweza kukupatia asali zaidi


Hii ni aina nzuri na rahisa sana ya mzinga. Pia hufahamika kama mzinga wa fremu, kwa kuwa ina fremu ambazo vichane vya masega hujishikiza. Pia una chumba kikubwa ambacho malkia hutagia mayai. Malkia anazuiliwa kuhama kwenda chumba kingine kwa kutumia waya. Kwenye chemba maalumu ya kutagia juu yake pana chemba ya kuhifadhia asali. Vichane vya masega vinatengezwa kwenye fremu na si kwenye nguzo kama ilivyo kwenye Top bar.
Ili kuvuna asali, mfugaji akiwa na masega yaliyojaa asali, hutumia vifaa maalum kwa ajili ya urinaji na kuhifadhi asali bila kupata tabu.


Langstroth ni gali kiasi fulani kwani huuzwa kuanzia kiasi cha TSh 70,000. Unaweza kuipata kutoka katika taasisi zilizopo hapo chini, taasisi na karakana binafsi, au wakala wa Serikali.
Chanzo: Mkulima Mbunifu

Nyanya zinahitaji matunzo ili upate mavuno

Mkulima atapata faida kubwa ikiwa atatunza zao la nyanya kwa uangalifu mkubwa.



Nyanya huzaa vizuri sana hasa zinapowekewa mbolea mboji au samadi iliyooza vizuri. Unaweza kuongeza mbolea ya minjingu kiasi cha kijiko kimoja cha chakula au vijiko 3 vya chai kwa kila shimo. Endapo ardhi ina upungufu wa mbolea asili, inashauriwa kupanda kwanza mimea yenye uwezo wa kutoa mbolea vunde bora kama vile kunde, mucuna, soya au clotalaria kabla ya kusia mbegu za nyanya au kupanda. Epuka mbolea za viwandani kwa kuwa nitrojeni ikizidi husababisha nyanya kuvimba, na baadaye kuoza kirahisi, pia husababisha mnyanya kukua kupita kawaida. Kuwa na nitrojeni iliyozidi kwenye udongo pia husababisha majani kuwa laini sana hivyo kuvutia wadudu na magonjwa kirahisi. Ushindani wa magugu dhidi ya nyanya zako unakuwa ni mkubwa sana, hasa sehemu zenye joto na unyevu mwingi.


Ili kudhibiti magugu kwenye eneo lililo wazi, fyeka mara kwa mara na uhakikishe kuwa ni mafupi kuliko nyanya mpaka hapo nyanya zitakapokomaa na kuiva. Acha magugu uliyofyeka kwenye shamba lako yawe kama matandazo ili kusaidia kupunguza au kuzuia mmomonyoko wa ardhi, kupunguza joto kwenye ardhi na kuhifadhi unyevu kwenye udongo. Hii inaweza pia kufanywa kwa kupalilia kwa mikono katikati ya mistari ya nyanya, na kuweka matandazo hayo katikati ya mistari.


Fito


Kwa aina ya nyanya zinazorefuka sana, chomeka walau fito zenye urefu wa mita 2 katika kila mche wa nyanya na ufungie kwa kutumia kamba. Badala yake unaweza kutengeneza kichanja chenye nyaya na nguzo kila baada ya mita 1 au 2 na nyingine yenye urefu wa mita 0.15 kutoka ardhini. Funga kamba imara kwa kila mnyanya. Mnyanya unaweza kuzungushwa kwa uangalifu mkubwa kwenye kamba hiyo kulingana na unavyokuwa.


Kukatia matawi ni muhimu sana kwa aina zote za nyanya. Unaweza kuacha shina kukua na kukata matawi mawili ya awali ili kuruhusu mmea kukua vizuri. Kata matawi kulingana na mmea unavyokuwa kwa wiki. Mmea unapokuwa na viriba 6 au 8 vya maua ni vizuri kukata kichwa ili kuwezesha ukuaji mzuri matunda yatakayotokea ambayo yatakuwa na soko zuri. Majani yaliyo karibu na ardhi ni lazima yaondolewe ili kusaidia kuzuia uwezekano wa mabaka kuingia kwenye mmea na matunda. Hakuna kanuni za kukata matawi au kupata idadi flani ya matunda kwa kila mmea, hii inategemeana na mkulima na aina ya nyanya.  Nyanya zinahitaji umwagiliaji mzuri katika siku za mwanzo toka kupandwa, wakati wa kuchanua, na wakati wa kukuza matunda. Kupatikana kwa maji ya kutosha kwenye minyanya, husaidia kwa kiasi kikubwa kuwa na mazao na kukomaa kwa wakati mmoja.  Husaidia pia kupunguza uwezekano wa kuvimba na kuoza kwa nyanya, muonekano usiokuwa wa kawaida hutokana na ukosefu wa kalishamu ya kutosha wakati wa kutengeneza na kukuza matunda. Wakati wa kiangazi, ni muhimu kunyweshea angalau mara mbili kwa wiki. Unyeshaji kwa njia ya matone ni njia bora zaidi na isiyokuwa na madhara ukilinganisha na umwagiliaji wa mifereji, hii ni kwa sababu maji hudondoka kidogo kidogo kwenye shina.


Kuvuna


Nyanya kwa ajili ya kuuza zinaweza kuvunwa zikiwa bado na rangi ya kijani baada ya kukomaa, kisha zinaweza kuiva zikiwa zinasafirishwa kwenda sokoni, au zikahifadhiwa kwanza ili ziive. Nyanya zinazotumika kwa ajili ya kutengeneza supu, juisi, na mchuzi huachwa shambani mpaka ziive kiasi cha asilimia 85. Nyanya huchumwa zikiwa bado ngumu, lakini kiasi cha asilimia 65 huwa tayari kuchumwa kwa wakati mmoja.


Wadudu wa nyanya na njia za asili za kudhibiti


Sota (cutworms)


Hawa ni wadudu hatari wanaoshambulia vitalu vya nyanya. Wanakata shina la mimea iliyooteshwa au inayoota.


Ni nini cha kufanya;


• Ondoa magugu mapema, angalau wiki mbili kabla ya kupanda.
• Chimbua na utifue vizuri shamba lako kabla ya kupanda. Hii inasaidia kuwaibua sota na kufanya waliwe na maadui zao.
• Tengeneza wigo kulinda miche iliyohamishwa na kupandwa shambani. Wigo unaweza kutengenezwa kwa kuzungushia karatasi, karatasi ya foili, au ubao mwepesi kuzunguka sehemu ya bustani.
• Chimba karibu ya mimea iliyoharibiwa na uwateketeze sota.
• Wahifadhi wadudu wa asili wanaokula sota.


Vidukari (Aphids)



Vidukari hunyonya maji kwenye mimea na kusababisha mimea kupunguza uwezo wa kukua, pia hutoa ute kama asali, ambao husababisha unga unga unaosababisha mimea kukakamaa. Unga huu kwenye matunda husababisha yasipate soko.


Ni nini cha kufanya;


• Tunza wadudu wa asili wanaokula vidukari. Epuka kutumia madawa kwa wingi kwani yanaweza kuua wadudu wa asili wanaodhibiti vidukari.
• Tumia matandazo yanayong’aa. Vitu vinavyo akisi mwanga kama vile aluminiamu, husaidia vidukari wasiwezi kutua kwenye mimea.


Minyoo – (Root-knot nematodes)


Root knot huathiri sana nyanya.  Madhara yanakuwa makubwa zaidi sehemu yenye udongo wa kichanga na kunyeshea kwa kutuamisha maji. Minyoo husababisha vifundo kwenye mizizi. Mimea iliyoathiriwa hunyauka, na wakati mwingine hufa kabisa wakati wa jua.


Ni nini cha kufanya;


• Fanya mzunguko wa nyanya na nafaka.
• Usiweke kitalu cha miche mahali ambapo unahisi kuwepo magonjwa.
• Tumia aina ya nyanya inayostahimili magonjwa.
• Panda mazao mseto.
• Hakikisha kuna kiasi cha kutosha cha mbolea asili kwenye udongo.
Chanzo: Mkulima Mbunifu

Pandikiza parachichi upate mavuno zaidi

Msukumo wa uhitaji mkubwa wa parachichi kwa wingi na zenye ubora unawasukuma wakulima kutumia teknolojia mpya.



 
Upandikizaji hujumuisha aina mbili za mimea. Unachukua mmea mmoja ambao unadhani hauna tija nzuri, na sehemu ya mmea mwingine ambao una ubora zaidi na kupandikiza kwa kukata na kufunga pamoja ili kupata mbegu bora zaidi. Utaratibu wa kupandikiza hivi sasa umekuwa silaha ya wakulima kuwakomboa dhidi ya wadudu pamoja na magonjwa, na hili kwa sasa halifanyiki tena maabara kama ilivyokuwa awali na hii inadhibitishwa na yale tuliyojionea Njombe tulipotembelea wakulima.


 
Kwenye shamba la bwana Bosco Kidenya, ana kitalu chenye zaidi ya miche 1200 ya miparachichi, baadhi ikiwa tayari imeshapandikizwa na mingine ikiwa inasubiri kufikia wakati wa kupandikiza.  Huyu ni mmoja kati ya wakulima walio wengi wanaofanya kazi kwa karibu na CARITAS Njombe, kuboresha uzalishaji wa parachichi, pamoja na kuboresha kipato cha wakulima ambao wanazalisha matunda na mboga mboga.


Mbinu wanayotumia


Wakulima hukusanya kokwa za parachichi kutoka maeneo ya sokoni; wanachofanya ni kuhakikisha tu kuwa mbegu hiyo ni safi, haijaathiriwa na magonjwa na itaota. Baada ya hapo huchagua zile zenye muundo mzuri na kuzipanda kwenye boksi au kwenye sehemu ya kitalu. Baada ya kuota huziotesha kwenye makopo, au kwenye viriba kisha kuendelea kumwagilia maji mpaka zinapokuwa na umbo usawa wa penseli. Upandikizaji ni lazima ufanyike wakati mmea umefikisha unene wa penseli. Kupandikiza kwa kutumia chipukizi lililolingana na mche unaopandikizia ni njia yenye mafanikio zaidi.


Upandikizaji ni lazima ufanyike wakati ambao mizizi bado ni laini. Pandikizi litakalotumika wakati wa kupandikiza ni lazima lisiwe katika hatua ya ukuaji kwa wakati huo, na ni lazima umbo liwiane na mti linapopandikizwa kuzuia maji yasipotee na kusababisha pandikizi kukauka.


 
Mapandikizi ni lazima yatokane na aina ya parachichi ambazo zimeboreshwa kama vile hass, fuerte  au puebla. Kwa wale wakulima ambao mmea utatoa majani mapya. wana mkataba na Africado, watahitajikupata mapandikizi kutoka kwenye miti ya hass. Hii ina maanisha kuwa mkulima anayetaka kuanzisha kitalu kwa ajili ya kupandikiza ni lazima apande walau miti 5 ya parachichi aina ya hass ili kupata mapandikizi.


Njia ya kupandikiza ina ufanisi zaidi na ni rahisi kuliko kupanda miche upya, kwa kupandikiza inagharimu chini ya asilimia 75, kuliko kupanda miche upya na kuweza kupata aina ambayo inastahimili magonjwa. Wakulima pia wamekuwa na rikodi nzuri ya ongezeko la mavuno kutokana na mimea waliyopandikiza, pamoja na upungufu wa matumizi ya madawa.


Wakulima ambao wanafanya kazi zao chini ya CARITAS Njombe sasa wanaona faida kubwa inayotokana na kupandikiza, wameamua kuwekeza kwenye utaalamu huu na kuwa na miche mingi kwenye vitalu vyao. Hii ni mbinu ya kilimo ambayo ina faida kubwa kwa mkulima, huku akiwa amewekeza kwa kiasi kidogo sana katika kukabiliana na wadudu na magonjwa na kuepuka kuwa na mazao yenye ubora wa chini.



Namna ya kupanda


Nafasi halisi inayohitajika na mmea wa parachichi ili ukae vizuri ni nafasi ya 9m x 9m. Chimba shimo katika vipimo vya 60sm x 60sm kwa 60sm kwenda chini kisha tenga udongo wa juu na wa chini. Changanya udongo wa juu na mbolea ndoo moja iliyooza vizuri, pamoja na kiganja kilichojaa cha mbolea ya minjingu.


Ondoa mche wako kwenye kiriba ulipopandwa. Hii itakuwa rahisi zaidi endapo ulikuwa umenyweshea muda kidogo uliopita. Panda kwa kutumia udongo wa juu uliochanganya na mbolea na uweke mpaka kujaza shimo.


Mwagilia maji mara baada ya kupanda. Funika mmea mchanga kwa kutumia majani ya migomba au aina nyingine ya majani yanayofanana na hayo, mpaka kufikia kipindi ambacho mmea utatoa majani mapya.

Utunzaji wa udongo kwa ajili ya kilimo hai

Uelewa wa maisha ya mimea husaidia kwa kiasi kikubwa kwa hatua ya kuchukua kuilisha mimea hiyo.


 
Utunzaji wa udongo unategemeana kwa kiasi kikubwa na mazingira ya kibiolojia. Kazi kubwa ya baadhi ya viumbe hai waliomo kwenye udongo, ni kumeng’enya mabaki ya mimea na viumbe hai wengine. Mtiririko huu hufanya uwepo wa nguvu, virutubisho, na hewa ya kaboni, ambavyo kwa pamoja hutengeneza rutuba kwenye udongo.


Utunzaji wa rutuba ya udongo unaongozwa na filosofia hii ‘Lisha udongo ili nao ulishe mimea.’ Udongo wenye rutuba utazalisha mimea yenye afya inayoweza kukabiliana na magonjwa. Uzalishaji wa mazao kwa njia za asili uhakikisha kunakuwepo uzalishaji wa kutosha bila ya kutumia pembejeo za ziada isipokuwa matandazo, mboji na bila kutifua udongo mara kwa mara. Ongezeko la malighafi za asili husaidia kuimarisha udongo na kufanya kuwepo kwa virutubisho vya kutosha.


Athari kwa afya ya mimea


Kwa bahati mbaya, aina ya kilimo cha kisasa na kinachotumia kemikali hufanywa tofauti na ilivyo kwa kilimo hai. Katika aina hii ya kilimo; udongo hulimwa mara kwa mara jambo linalosababisha uharibifu wa muundo wa udongo, uwiano wa virutubisho, ambapo virutubisho huongezwa kwa kutumia mbolea za viwandani na matandazo hayazingatiwi. Muundo wa udongo unapobadilika, rutuba nayo hupungua, uwezo wa udongo kwenye udongo pia hupungua.


Kiwango cha udongo mzuri pia hupungua kwa kuwa hakuna tena viumbe hai wanaotengeneza udongo ila unapungua kila msimu wa mavuno. Kwa asili mzunguko huu huwa na matokeo yanayoishia kwenye afya ya mimea, na hapa wadudu huchukua nafasi inayowawezesha kufikia malengo yao.


Ziba pengo


Wakulima wanatakiwa kuhakikisha kuwa kuna virutubisho vya kutosha shambani mwao kila wakati. Ikiwa kuna mwanya pale ambapo baadhi ya pembejeo zinakosekana, kununua virutubisho kwa ajili ya udongo vilivyomo kwenye mfumo wa mbolea za asili inaruhusiwa. Hata hivyo, weka utaratibu wa kuwa na virutubisho kutoka shambani mwako muda wote.


Endapo tukitegemea kulisha udongo kutokana na mbolea za viwandani na kutumia virutubisho vya asili, bado tutakuwa tunafanya sawa na yanayofanyika katika kilimo cha kisasa. Tutakuwa hatujauongezea udongo uwezo wa kujitengeneza na kuongezeka, jambo ambalo ndio msingi muhimu wa kilimo hai.


Vyanzo vya virutubisho


Mimea inayofunika udongo – Mimea inayotambaa huongeza na kushika virutubisho kwenye udongo, kuongeza malighafi zinazooza kwenye udongo, kuzuia madini ya naitraiti kuzama kwenye udongo, virutubisho kutiririshwa, na mmomonyoko wa udongo. Jambo la muhimu hapa ni kuwa udongo umefunikwa ili kuzuia uharibifu. Mimea jamii ya mikunde inapendekezwa zaidi kwa kuwa
husaidia kuongeza nitrojeni kwenye udongo inayopatikana hewani.


Inashauriwa pia kuchanganya mimea jamii ya mikunde na nyasi kwa kuwa nyasi hutumia nitrojeni nyingi sana kutoka kwenye udongo, hivyo itasaidia kutokuharibika kwa mtiririko mzima wa uwekaji wa nitrojeni kwenye udongo.


Mboji - Mboji hasa inayotengenezwa kwa kutumia kinyesi cha wanyama, inaweza kuwa chanzo kizuri cha viumbe wadogo kwenye udongo na virutubisho vyenye gharama ndogo. Unapotumia mboji, changamoto kubwa ni kuhakikisha kuwa imeoza vizuri na namna ya kuitumia kwa usahihi. Endapo mchanganyiko uliotumika kutengeneza mboji hiyo yalikuwa na ubora wa chini, basi mboji hiyo nayo itakuwa na ubora mdogo sana. Itakuwa vizuri kama wakulima hawataacha mboji ikapigwa na jua au mvua, kwa kuwa hali hii inaweza kusababisha kupotea kwa virutubisho kwenye mboji. Kinyesi cha mifugo huboresha mboji zaidi.


Utafiti wa hivi karibuni unaonesha kuwa kiasi cha 15% ya virutubisho vinavyopatikana kwenye mboji hutumika shambani kwa mwaka wa kwanza. Hivyo, matumizi ya mara kwa mara ya mboji yanapendekezwa ili kuweza kuongeza nitrojeni na malighafi zinazo oza kwenye udongo.


Samadi - Samadi inayotokana na wanyama waliokomaa inaweza kuwa na uwiano mzuri wa virutubisho vya nitrojeni na aina nyingine kwa kiasi kidogo. Tatizo moja la samadi ni upatikanaji pamoja na kutokuwa na ubora unaofanana wakati wote. Kiasi kikubwa cha samadi inayotumika kwenye shamba la mboga, huozeshwa kabla ya kutumika, jambo linalosaidia kupunguza madhara kwenye vyakula.


Malengo kwa ajili ya udongo na mazao
•  Kuongeza malighafi zinazo oza kwenye udongo
• Kuboresha muundo wa udongo
• Kuwezesha upatikanaji wa nitrojeni
• Kuongeza uwezo wa uhifadhi wa rutuba
• Kujenga uwepo wa uhai wa viumbe hai kwenye udongo
• Kufifisha magonjwa ya mazao
• Kujenga mazingira ya udongo wenye uwiano

Chanzo: Mkulima Mbunifu

Sunday, March 17, 2013

Wizara Kufufua Mifumo Asili ya Kilimo



Mfumo wa Kilimo cha asili aina ya Kiamba unaotumiwa na kabila la Wachaga.

Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika imeanzisha Mradi wa kufufua Mifumo muhimu ya asili ya kilimo Duniani (Global Importance Agricutural Heritage System- GIAHS) ili kuendeleza Kilimo cha asili (Oranic Farming) na kumpunguzia mkulima gharama za uzalishaji.
Mradi huo unatekelezwa na Shirika la chakula Duniani (FAO) ambao unalenga kutambua mifumo ya asili na endelevu ya kilimo na ufugaji ili kumsaidia mkulima.
Afisa Mkuu wa Kilimo kutoka Idara ya Matumizi Bora ya Ardhi Bw.  Firmat Banzi
alisema mradi unagharimu zaidi ya dola laki mbili ambazo zimetolewa na Serikali ya Ujerumani.

Alisema kuwa katika Afrika Mashariki nchi ya Tanzania na Kenya ilichaguliwa kufufua mifumo hiyo kwa kuwa na sehemu muhimu za kilimo zanazotumia mifumo hiyo.
Aliongeza kuwa baada ya kuchanguliwa nchi ya Tanzani ilipendekeza mifumo mitatu ya kilimo asili ambayo ni Kihamba ambao hutumiwa na wachaga, Ndiva wa Wapare na Ngoro ambao hutumiwa na kabila la wamatengo.
Alifafanua kuwa mifumo hiyo mitatu ilifanyiwa utafiti na baadaye mfumo wa kichanga ulichaguliwa na kuanza kutumika. 
Aidha, alisema kijiji cha Chimbe juu kilichopo wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro ndio kilichonufaika na mradi huo na sasa unafikia hatua ya mwisho katika utekelezaji wake.
Hatua hiyo imekuja baada ya tafiti mbalimbali kuonesha kushuka kwa bei ya zao la kahawa na kusema kuwa kilimo asili huongeza bei za mazao kwa kuwa mazao yanayolimwa hayatumii kemikali na badala yake hutumia mbolea ya asili kama vile samadi, aliongeza Bw. Banzi.
Mradi huo utasaidia kuboresha zao la kahawa kwa kutumia mbinu husishi za  kukabiliana na wadudu waharibifu wa mazao.
Alifafanua kuwa  mradi unajumuisha utayarishaji wa vitalu vya miche, ukarabati wa mifumo asili ya umwagiliaji na utayarishaji wa mbolea za asili kama vile samadi.
Ili kuhakikisha mradi huu unaendelea Bw. Banzi alisema wameshirikisha wadau mbalimbali ambao watasaidia kuangalia kwa karibu maendeleo ya mradi, alitaja wadau hao kuwa ni Chama cha Ushirika KNCU cha Kilimanjaro pamoja na halmashauri ya wilaya.
Mifumo ya asili ya kilimo ilianza kupendekezwa dunia toka mwaka 2002 na baadhi ya nchi zimeanza kutumia mifumo hii, baadhi ya nchi hizo ni Japani, Philipino, China na Ujerumani.

Mifumo ya Asili ya Kilimo Kuendelezwa Kuinua Kilimo

Mazao yaliyostawi vizuri yakionyesha mojawapo ya aina ya kilimo Asili cha Mseto
Wadau wa kilimo, sera, mazingira, utawala, na mashirika ya kimataifa, wametoa wito wa kubaini mifumo asili ya Kilimo kwa kutambua mchango katika uhakika wa chakula na kipato.
Wito huo ulitolewa katika warsha iliyofanyika jijini Dar es Salaam iliyojumuisha wadau hao ili kutathmini mchango wa mifumo asili ya kilimo na changamoto zilizopo ili kuiboresha na kiendeleza.
Ilibainika kuwa Tanzania ina mifumo mingi ya asili ya kilimo na mifugo ambayo imedumu kwa taribani zaidi ya miaka 100 hadi 700.
Katika kipindi hicho, mifumo mingi imekumbana na mabadiliko ya hali ya hewa lakini imekabili na kudumu, hii inaonyesha kuwa kuna vitu vingi vya kujifunza katika mifumo hiyo.
Aidha, wadau wamependekeza mifumo ya asili ya kilimo na ufugaji kuingizwa katika sera kati ya zilizopo ili ipate nguvu ya kusimamiwa na kuendelezwa hasa ikizingatiwa umuhimu wake katika kuimarisha usalama wa chakula na kipato kwa kaya na taifa kwa ujumla.

Pia wametaka mashirika ya kimataifa yaendelee kuchangia kwa rasilimali uendelezaji wa mifumo asili endelevu kwani manufaa yake ya mazingira ni ya ulimwengu.

Afisa Mkuu wa Kilimo kutoka Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Firmat Banzi alisema kuwa mifumo asili ya kilimo ina haja ya kuendelezwa ili kuboresha na kuimarisha maarifa asili kuwezesha ushiriki wa wakulima katika utunzaji wa mifumo hiyo.
Alifafanua kuwa uendelezaji wa mifumo hiyo utawapa fursa wakulima kuweza kushiriki kikamilifu katika kilimo wakiwa na uhakika wa kupata mazao mengi kuweza kujitosheleza kwa chakula na kujiongezea kipato pamoja na kuboresha hifadhi ya mazingira hasa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
Washiriki kwa pamoja wamepitisha azimio linalotambua mchango wa mifumo ya asili ya kilimo na ufugaji na wametoa wito wa kubaini mifumo asili iliyopo nchini, kutathmini mchango wake na changamoto kwa lengo la kuiboresha na kuiendeleza.

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU BEI ZA VYAKULA MIKOANI



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIAWIZARA YA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA


TAARIFA KWA UMMA  KUHUSU BEI ZA VYAKULA MIKOANI


UTANGULIZI: 

Tulianza msimu huu 2012/13 tukiwa na ziada kidogo ya chakula na kwa kujitosheleza kwa asilimia 113. Msimu huu, tofauti na msimu uliopita hatukuzuia wakulima na wafanyabiashara kuuza mazao yao nje ya nchi.

Pamoja na uzalishaji tuliokuwa nao katika maeneo kadhaa ya nchi kulikuwepo na maeneo ambayo uzalishaji wake haukuwa wa kuridhisha kutokana na hali mbaya ya hewa na hivyo kuwa na upungufu wa chakula.  Upungufu huu unajidhihirisha kutokana na kupungua  kwa uingiaji na upatikanaji wa vyakula sokoni, hususani unga wa mahindi ambacho ni chakula kikuu        na  bei ya soko kupanda  sana kwa viwango vilivyo juu ya bei ya wastani nchini.

Uchambuzi wa bei za vyakula unaonesha kwamba bei ya wastani ya mahindi kitaifa ni shilingi 675 kwa kilo.  Aidha, bei ya mahindi katika masoko ya miji mkuu ya baadhi ya mikoa iko juu ya wastani.  Kwa mfano, bei ya Dar es Salaam tarehe 28 Novemba, 2012 ilifikia shilingi 750 kwa kilo, Mwanza shilingi 825, Moshi shilingi 700, Tanga shilingi 785, Tabora shilingi 750 na Mtwara shilingi 735.  Aidha, unga wa sembe uliuzwa kati ya shilingi 1,100 na shilingi 1,500 kwa kilo, mwezi Desemba 2012.

Hali ilivyo katika maeneo mengi ya nchi ni kwamba, viwango vya upatikanaji wa chakula vinatofautiana katika maeneo mbali mbali.  Wakati mikoa minane (8) ya Iringa, Rukwa, Mbeya, Kagera, Mtwara, Kigoma, Ruvuma na Morogoro ilikuwa na ziada ya chakula, mikoa saba (7) ya Pwani, Mara, Tanga, Lindi, Mwanza, Singida na Dodoma ilikuwa na hali ya utoshelevu tu na mikoa sita (6) ya Shinyanga, Tabora, Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Dar es Salaam ilikuwa na uhaba wa chakula.

Kutokana na upungufu wa chakula kuzidi kujitokeza, mwezi Oktoba, 2012, Serikali, kupitia Kamati ya Maafa iliidhinisha mgao wa tani 18,417.8 wa chakula cha njaa kutoka katika maghala ya Hifadhi ya Chakula ya Taifa (National Food Reserve Agency) kwenda katika Halmashauri 35 za mikoa 12 zilizobainika kuwa na upungufu mkubwa wa chakula.  Mikoa iliyopewa chakula cha njaa ni Arusha, Dodoma, Kilimanjaro, Lindi, Mara, Manyara, Morogoro, Mwanza, Shinyanga, Singida, Tabora na Tanga.

Kutokana na hali ya upungufu wa chakula kuzidi kuendelea na kujitokeza kwa majanga mengine kama mafuriko, Serikali iliidhinisha mgao wa nyongeza ya chakula hadi kufikia tani 26,958.300 kwa Halmashauri zilizokuwa  na mahitaji makubwa ya chakula cha msaada.  Aidha, upungufu wa chakula katika baadhi ya maeneo yanayozalisha nafaka kwa wingi umesababisha kupungua kwa chakula kinachosambazwa katika soko hivyo kufanya usambazaji wa chakula kutolingana na mahitaji ya soko. Hali hii imesababisha kupanda kwa bei ya mahindi na unga wa  mahindi katika baadhi ya masoko hususan  ya mijini. Ili kukabiliana na hali hiyo Serikali imechukua  hatua zifuatazo:-
(i)      Kutoa chakula cha msaada kwa maeneo yaliyokuwa na upungufu wa chakula.
Kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu wenye upungufu wa chakula Serikali iliendelea kuongeza mgao wa chakula cha msaada kutoka tani 18,417.8 hadi kufikia  tani 28,250.300. Hadi kufikia mwezi Januari, 2013 jumla ya tani 19,040.865 za mahindi zilishachukuliwa. Aidha, jumla ya tani 9,209.435 bado hazijachukuliwa na mikoa iliiyopewa mgao wa nyongeza. Mikoa ambayo bado haijachukua nyongeza hiyo ni Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Tabora, Mbeya na Mara. Kiambatisho Na. 1
(ii)    Kuuza tani 40,000 za mahindi kutoka kwenye ghala la Taifa kwa ajili ya kushusha bei ya unga wa mahindi.

Serikali imeidhinisha kuuzwa tani 40,000 za mahindi kutoka katika ghala la chakula la taifa ambapo tani 20,000 zitauzwa kati ya mwezi Januari na Februari, 2013. Kwa bei ya shilingi 450 tu kwa kilo. Kiasi kingine cha tani 20,000 kilichobaki kitauzwa kuanzia mwezi Machi katika maeneo yatakayobainika kuwa na upungufu wa chakula na bei kuendelea kupanda. Mgao Kimkoa ni kama inavyoonyesha kwenye Kiambatisho Na. 2.

2.        UTARATIBU WA KUUZA MAHINDI KWA WASAGISHAJI
Mikoa yenye bei ya mahindi iliyo juu ya bei ya wastani kitaifa ndiyo iliyopewa mgao. Mikoa hiyo na mgao wake katika mabano ni kama ifuatavyo:  Arusha (tani 1100), Dodoma (tani 400), Kilimanjaro (tani 400), Lindi (tani 400), Mara (tani 900) , Manyara (tani 800), Morogoro (tani 400), Mwanza (tani 2500), Shinyanga (tani 1029), Singida (tani 500), Tabora (tani 1000), Tanga (tani 700), Mtwara (tani 600) , Pwani (tani 700), Simiyu (tani 1971) na Dar es Salaam (tani 6400).
Utaratibu unaotumika kuuza mahindi kwa wasagishaji ni kama ifuatavyo:
  i.        Mikoa imeelekezwa kuteua wasagishaji waaminifu wenye nia na uwezo wa kusagisha unga kwa ajili ya kuuza kwa walaji kwa bei elekezi iliyopangwa na mkoa ambayo ni kati ya shilingi 750 hadi 900 kwa kuzingatia gharama za usafirishaji.
 ii.        Wasagishaji walioteuliwa wanatakiwa kukidhi vigezo vilivyowekwa kama vile, uwezo wa kulipa fedha za mahindi ndani ya muda uliopangwa, uwezo wa kuhifadhi kiasi cha mahindi anachonunua, uwezo wa kusagisha, kufungasha na kusambaza unga ndani ya siku saba kuanzia siku aliyochukua mahindi, pamoja na kukubali kuuza kwa bei elekezi.
iii.        Wasagishaji walioteuliwa na mikoa watapewa vibali na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula ili waweze kununua mahindi kutoka katika maghala ya Wakala kama watakavyopangiwa.
iv.        Mikoa itaingia mikataba na wasagishaji walioteuliwa na kusimamia utekelezaji wa mikataba hiyo ili kuhakikisha mpango huu unatekelezwa kwa ufanisi na unaleta manufaa yaliyokusudiwa.


v.        Mikoa itachukua hatua kwa msagishaji ambaye atabainika kutumia vibaya kibali alichopewa, kama vile kuuza kibali hicho kwa msagishaji mwingine, kusafirisha na kuuza mahindi au unga kwenye maeneo tofauti na aliyopangiwa, kutosagisha na kuuza unga ndani ya siku saba kwa mujibu wa mkataba.
3.   UTEKELEZAJI WA MPANGO WA KUPUNGUZA BEI YA UNGA KWA WALAJI
Mikoa iliyopewa mgao imeelekezwa utaratibu wa kununua mahindi kutoka katika maghala ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula. Hadi kufikia tarehe 14 Januari, 2013 jumla ya mikoa 11 kati ya Mikoa 16 ilikuwa imewaslisha orodha ya wasagishaji kwa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula. Mikoa hiyo ni Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Singida, Dodoma, Morogoro, Lindi, Mtwara, Pwani,Tanga na Dar es Salaam. Mikoa ambayo haijawasilisha orodha ya wasagishaji ni Mwanza, Tabora, Shinyanga, Mara. 

Kuendelea kuchelewa kuwasilisha orodha ya wasagishaji kunasababisha kuchelewesha zoezi zima la utoaji wa mahindi, usafirishaji, usagishaji na hivyo kuchelewesha unga kuingia sokoni hali inayosababisha bei kuendelea kupanda.  Mikoa hiyo inaagizwa kuwasilisha orodha ya wasagishaji ndani ya siku saba kuanzia sasa.  Jumla ya wasagishaji 127 tayari wameshapewa vibali vya kununua mahindi yanayofikia tani 12,520.00 ambapo tani 7,858.291 zimeshalipiwa na uchukuaji unaendelea lakini kasi ya kulipia na kuchukua ni ndogo. Orodha ya Wasagishaji kama ilivyowasilishwa na mikoa na kiasi walichoidhinishiwa kununua imeoneshwa katika Kiambatisho Na.3.

Serikali inawaagiza Wasagishaji wote waliopewa vibali vya kununulia mahindi kuhakikisha wanalipia na kuchukua kiasi chote cha mahindi kama walivyoidhinishiwa katika vibali vyao ndani ya siku saba kuanzia sasa, vinginevyo Serikali italazimika kufuta vibali hivyo na kuvigawa upya kwa Wasagishaji wengine katika mikoa husika wenye nia thabiti ya kufikisha unga sokoni.
4.  USIMAMIZI NA UFUATILIAJI WA UTEKELEZAJI
Wakuu wa Mikoa  na Wilaya wanaagizwa kusimamia na kufuatilia kikamilifu utekelezaji wa zoezi hili kama ilivyoelekezwa. Aidha, mikoa inatakiwa kuweka mfumo mzuri wa usimamizi na usambazaji wa unga unaotokana na mahindi yaliyonunuliwa kutoka katika ghala la Serikali ikiwa ni pamoja na kuwafahamisha wananchi maeneo ambayo unga huo unapatikana pamoja na bei elekezi iliyopangwa na mikoa.
Katika ngazi ya Taifa Serikali, kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu imeandaa utaratibu wa kufuatilia utekelezaji wa mkakati huu katika mikoa yote iliyopata mgao wa chakula cha njaa au mgao ulitolewa kwa wasagishaji kwa ajili ya kupunguza bei ya unga katika masoko ya mijini.
5. MWISHO
Kwa kuwa maghala ya Dar es Salaam (Kipawa), Arusha, Dodoma na Shinyanga yana upungufu wa akiba ya chakula kulinganisha na mahitaji ya sasa katika maeneo hayo,  Serikali inaendelea kuhamisha chakula kutoka katika maghala yenye akiba ya kutosha kwenda katika maghala yenye upungufu ili kurahisisha usambazaji wa chakula katika maeneo yenye upungufu. Tunaendesha zoezi hili la kuhamisha  chakula kwa kutumia Shirika la Reli (TRL) , Jeshi la Wananchi na wasafirishaji binafsi ili kuhakikisha kwamba chakula kinafika haraka.

Tuesday, October 16, 2012

AGRICULTURE AND ENTERPRISES SKILLS FOR WOMEN SMALLHOLDERS PROJECT BY FASO


Women on their farms

Women now make up the majority of the agricultural sector in Tanzania, but recent evidence suggests that not only is their productivity constrained by a lack of appropriate skills training , but also that they are particularly vulnerable to a range of changes including economic and environmental changes. Equipping women on small farms with the skills to improve production and manage change is therefore an important step towards securing livelihoods and reducing poverty. Lack of credit and capital, insecure land tenure and inadequate rural infrastructure make the application of new agricultural and enterprise strategies risky for women smallholders. FASO can play an important role in mitigating these risks by facilitating access to credit, helping women manage capital, working towards more secure land tenure, and helping women lobby local government for the provision of better infrastructure.Training is best approach FASO will use to empower women in agriculture and enterprises development. Those skills will base on:-



Training in financial management
To run their businesses successfully, the women needed to be able to control and plan their finances. To do this, they needed to be able to price their goods, work out their profit margins, and understand when they were making a profit. The ability to price inputs (including the cost of labour), establish market prices, and understand the difference between income and profits, are important. FASO found that there important to deliver training designed to enable women, individually or in groups, to improve the financial management of their production: Training helps women to distinguish between personal money and business finances – individuals can take loans from business. They learn to make sure their debtors are not too many, to find reliable sources of credit, to manage their stock flows, and simple booking to manage their cash flows.

Training in marketing, packaging and pricing
In addition to financial management, smallholders also require marketing training. This was frequently noted in the interviews as one of the women’s most important concerns, well ahead of technical skills. Improving production techniques, although important, is not sufficient to create significant changes in their circumstances. Achieving more efficient production and increasing yields did not address one of the most serious problems for small producers, and especially women smallholders: their lack of market power. Problems with accessing markets forced women to sell their goods on disadvantageous terms, and prevented women reaping the full benefits of their work.

Training to support group organization
The appropriate training FASO will provide can support group organization. Groups need training and support at various points in their development in order to function effectively, and to have a chance to become self sufficient. FASO found that their groups had very similar needs in this area of:
  1. Training and guidance for group formation;
  2. Training in formulating constitutions and by-laws, decision making procedures and electing leaders, to enable the transparent regulation of the group; and
  3. Training in conflict management and leadership skills.
Training and guidance for group formation
The projects emphasized that groups that formed for the purposes of mutual support, as opposed to simply accessing credit, were more likely to operate successfully and have a better chance of ultimately becoming sustainable. Mostly of women started groups for three main reasons: socializing, access to savings and insurance, and changing practices and production

Training on access of credit in groups
A group approach (such as VICOBA) ensures that there is a collective responsibility for loans and reduces the individual risks. Project can play a valuable role in facilitating credit access for groups. It is important, however, that the initiative and responsibility for ensuring repayment remains with the group, as this is a key factor in ensuring the sustainability of credit access beyond the lifetime of a project. FASO Project will help groups to become more credit worthy by supporting proper group formation, and providing bookkeeping and literacy support.
FASO VICOBA Group training at Magereza, Moshi.

Training to enable transparent regulation of the group
The organizational training greatly improved the operation of the groups, and enabled them to make better use of their resources. Training in group management processes, such as establishing group regulations, leadership structures, and decision-making procedures, improved accountability within the group and reduced the potential for conflict between the executive and other members.

Training in conflict management and leadership skills
Training in how to discuss difficult topics with members and deal with challenging situations made the groups more stable and resilient, and therefore better able to achieve their goals over the long periods of time required.

 Benefits of enterprise training
The training can play an important role in helping prospective entrepreneurs become successful. For women, training in enterprise skills Is particularly valuable as they expanded into new areas. The entrepreneurship training is important in allowing producers in growth industries (including agriculture) to access more of the value chain associated with their product.
Women demanded a range of enterprise skills including bookkeeping, entrepreneurship and business management skills.
Developing the capacity of women and groups to take small, measured risks was both a major focus and a key challenge for each of the projects. While affecting this kind of change takes time, each project played an important role as a catalyst for this change.

IF YOUR A STAKEHOLDER ON AGRICULTURE, ENTERPRISES DEVELOPMENT, WOMEN EMPOWERMENT, etc CONTACT US FOR PARTNERSHIP TO IMPLEMENT THIS PROJECT..TOGETHER WE CAN!