Thursday, May 9, 2013

Utunzaji wa udongo kwa ajili ya kilimo hai

Uelewa wa maisha ya mimea husaidia kwa kiasi kikubwa kwa hatua ya kuchukua kuilisha mimea hiyo.


 
Utunzaji wa udongo unategemeana kwa kiasi kikubwa na mazingira ya kibiolojia. Kazi kubwa ya baadhi ya viumbe hai waliomo kwenye udongo, ni kumeng’enya mabaki ya mimea na viumbe hai wengine. Mtiririko huu hufanya uwepo wa nguvu, virutubisho, na hewa ya kaboni, ambavyo kwa pamoja hutengeneza rutuba kwenye udongo.


Utunzaji wa rutuba ya udongo unaongozwa na filosofia hii ‘Lisha udongo ili nao ulishe mimea.’ Udongo wenye rutuba utazalisha mimea yenye afya inayoweza kukabiliana na magonjwa. Uzalishaji wa mazao kwa njia za asili uhakikisha kunakuwepo uzalishaji wa kutosha bila ya kutumia pembejeo za ziada isipokuwa matandazo, mboji na bila kutifua udongo mara kwa mara. Ongezeko la malighafi za asili husaidia kuimarisha udongo na kufanya kuwepo kwa virutubisho vya kutosha.


Athari kwa afya ya mimea


Kwa bahati mbaya, aina ya kilimo cha kisasa na kinachotumia kemikali hufanywa tofauti na ilivyo kwa kilimo hai. Katika aina hii ya kilimo; udongo hulimwa mara kwa mara jambo linalosababisha uharibifu wa muundo wa udongo, uwiano wa virutubisho, ambapo virutubisho huongezwa kwa kutumia mbolea za viwandani na matandazo hayazingatiwi. Muundo wa udongo unapobadilika, rutuba nayo hupungua, uwezo wa udongo kwenye udongo pia hupungua.


Kiwango cha udongo mzuri pia hupungua kwa kuwa hakuna tena viumbe hai wanaotengeneza udongo ila unapungua kila msimu wa mavuno. Kwa asili mzunguko huu huwa na matokeo yanayoishia kwenye afya ya mimea, na hapa wadudu huchukua nafasi inayowawezesha kufikia malengo yao.


Ziba pengo


Wakulima wanatakiwa kuhakikisha kuwa kuna virutubisho vya kutosha shambani mwao kila wakati. Ikiwa kuna mwanya pale ambapo baadhi ya pembejeo zinakosekana, kununua virutubisho kwa ajili ya udongo vilivyomo kwenye mfumo wa mbolea za asili inaruhusiwa. Hata hivyo, weka utaratibu wa kuwa na virutubisho kutoka shambani mwako muda wote.


Endapo tukitegemea kulisha udongo kutokana na mbolea za viwandani na kutumia virutubisho vya asili, bado tutakuwa tunafanya sawa na yanayofanyika katika kilimo cha kisasa. Tutakuwa hatujauongezea udongo uwezo wa kujitengeneza na kuongezeka, jambo ambalo ndio msingi muhimu wa kilimo hai.


Vyanzo vya virutubisho


Mimea inayofunika udongo – Mimea inayotambaa huongeza na kushika virutubisho kwenye udongo, kuongeza malighafi zinazooza kwenye udongo, kuzuia madini ya naitraiti kuzama kwenye udongo, virutubisho kutiririshwa, na mmomonyoko wa udongo. Jambo la muhimu hapa ni kuwa udongo umefunikwa ili kuzuia uharibifu. Mimea jamii ya mikunde inapendekezwa zaidi kwa kuwa
husaidia kuongeza nitrojeni kwenye udongo inayopatikana hewani.


Inashauriwa pia kuchanganya mimea jamii ya mikunde na nyasi kwa kuwa nyasi hutumia nitrojeni nyingi sana kutoka kwenye udongo, hivyo itasaidia kutokuharibika kwa mtiririko mzima wa uwekaji wa nitrojeni kwenye udongo.


Mboji - Mboji hasa inayotengenezwa kwa kutumia kinyesi cha wanyama, inaweza kuwa chanzo kizuri cha viumbe wadogo kwenye udongo na virutubisho vyenye gharama ndogo. Unapotumia mboji, changamoto kubwa ni kuhakikisha kuwa imeoza vizuri na namna ya kuitumia kwa usahihi. Endapo mchanganyiko uliotumika kutengeneza mboji hiyo yalikuwa na ubora wa chini, basi mboji hiyo nayo itakuwa na ubora mdogo sana. Itakuwa vizuri kama wakulima hawataacha mboji ikapigwa na jua au mvua, kwa kuwa hali hii inaweza kusababisha kupotea kwa virutubisho kwenye mboji. Kinyesi cha mifugo huboresha mboji zaidi.


Utafiti wa hivi karibuni unaonesha kuwa kiasi cha 15% ya virutubisho vinavyopatikana kwenye mboji hutumika shambani kwa mwaka wa kwanza. Hivyo, matumizi ya mara kwa mara ya mboji yanapendekezwa ili kuweza kuongeza nitrojeni na malighafi zinazo oza kwenye udongo.


Samadi - Samadi inayotokana na wanyama waliokomaa inaweza kuwa na uwiano mzuri wa virutubisho vya nitrojeni na aina nyingine kwa kiasi kidogo. Tatizo moja la samadi ni upatikanaji pamoja na kutokuwa na ubora unaofanana wakati wote. Kiasi kikubwa cha samadi inayotumika kwenye shamba la mboga, huozeshwa kabla ya kutumika, jambo linalosaidia kupunguza madhara kwenye vyakula.


Malengo kwa ajili ya udongo na mazao
•  Kuongeza malighafi zinazo oza kwenye udongo
• Kuboresha muundo wa udongo
• Kuwezesha upatikanaji wa nitrojeni
• Kuongeza uwezo wa uhifadhi wa rutuba
• Kujenga uwepo wa uhai wa viumbe hai kwenye udongo
• Kufifisha magonjwa ya mazao
• Kujenga mazingira ya udongo wenye uwiano

Chanzo: Mkulima Mbunifu

Sunday, March 17, 2013

Wizara Kufufua Mifumo Asili ya Kilimo



Mfumo wa Kilimo cha asili aina ya Kiamba unaotumiwa na kabila la Wachaga.

Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika imeanzisha Mradi wa kufufua Mifumo muhimu ya asili ya kilimo Duniani (Global Importance Agricutural Heritage System- GIAHS) ili kuendeleza Kilimo cha asili (Oranic Farming) na kumpunguzia mkulima gharama za uzalishaji.
Mradi huo unatekelezwa na Shirika la chakula Duniani (FAO) ambao unalenga kutambua mifumo ya asili na endelevu ya kilimo na ufugaji ili kumsaidia mkulima.
Afisa Mkuu wa Kilimo kutoka Idara ya Matumizi Bora ya Ardhi Bw.  Firmat Banzi
alisema mradi unagharimu zaidi ya dola laki mbili ambazo zimetolewa na Serikali ya Ujerumani.

Alisema kuwa katika Afrika Mashariki nchi ya Tanzania na Kenya ilichaguliwa kufufua mifumo hiyo kwa kuwa na sehemu muhimu za kilimo zanazotumia mifumo hiyo.
Aliongeza kuwa baada ya kuchanguliwa nchi ya Tanzani ilipendekeza mifumo mitatu ya kilimo asili ambayo ni Kihamba ambao hutumiwa na wachaga, Ndiva wa Wapare na Ngoro ambao hutumiwa na kabila la wamatengo.
Alifafanua kuwa mifumo hiyo mitatu ilifanyiwa utafiti na baadaye mfumo wa kichanga ulichaguliwa na kuanza kutumika. 
Aidha, alisema kijiji cha Chimbe juu kilichopo wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro ndio kilichonufaika na mradi huo na sasa unafikia hatua ya mwisho katika utekelezaji wake.
Hatua hiyo imekuja baada ya tafiti mbalimbali kuonesha kushuka kwa bei ya zao la kahawa na kusema kuwa kilimo asili huongeza bei za mazao kwa kuwa mazao yanayolimwa hayatumii kemikali na badala yake hutumia mbolea ya asili kama vile samadi, aliongeza Bw. Banzi.
Mradi huo utasaidia kuboresha zao la kahawa kwa kutumia mbinu husishi za  kukabiliana na wadudu waharibifu wa mazao.
Alifafanua kuwa  mradi unajumuisha utayarishaji wa vitalu vya miche, ukarabati wa mifumo asili ya umwagiliaji na utayarishaji wa mbolea za asili kama vile samadi.
Ili kuhakikisha mradi huu unaendelea Bw. Banzi alisema wameshirikisha wadau mbalimbali ambao watasaidia kuangalia kwa karibu maendeleo ya mradi, alitaja wadau hao kuwa ni Chama cha Ushirika KNCU cha Kilimanjaro pamoja na halmashauri ya wilaya.
Mifumo ya asili ya kilimo ilianza kupendekezwa dunia toka mwaka 2002 na baadhi ya nchi zimeanza kutumia mifumo hii, baadhi ya nchi hizo ni Japani, Philipino, China na Ujerumani.

Mifumo ya Asili ya Kilimo Kuendelezwa Kuinua Kilimo

Mazao yaliyostawi vizuri yakionyesha mojawapo ya aina ya kilimo Asili cha Mseto
Wadau wa kilimo, sera, mazingira, utawala, na mashirika ya kimataifa, wametoa wito wa kubaini mifumo asili ya Kilimo kwa kutambua mchango katika uhakika wa chakula na kipato.
Wito huo ulitolewa katika warsha iliyofanyika jijini Dar es Salaam iliyojumuisha wadau hao ili kutathmini mchango wa mifumo asili ya kilimo na changamoto zilizopo ili kuiboresha na kiendeleza.
Ilibainika kuwa Tanzania ina mifumo mingi ya asili ya kilimo na mifugo ambayo imedumu kwa taribani zaidi ya miaka 100 hadi 700.
Katika kipindi hicho, mifumo mingi imekumbana na mabadiliko ya hali ya hewa lakini imekabili na kudumu, hii inaonyesha kuwa kuna vitu vingi vya kujifunza katika mifumo hiyo.
Aidha, wadau wamependekeza mifumo ya asili ya kilimo na ufugaji kuingizwa katika sera kati ya zilizopo ili ipate nguvu ya kusimamiwa na kuendelezwa hasa ikizingatiwa umuhimu wake katika kuimarisha usalama wa chakula na kipato kwa kaya na taifa kwa ujumla.

Pia wametaka mashirika ya kimataifa yaendelee kuchangia kwa rasilimali uendelezaji wa mifumo asili endelevu kwani manufaa yake ya mazingira ni ya ulimwengu.

Afisa Mkuu wa Kilimo kutoka Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Firmat Banzi alisema kuwa mifumo asili ya kilimo ina haja ya kuendelezwa ili kuboresha na kuimarisha maarifa asili kuwezesha ushiriki wa wakulima katika utunzaji wa mifumo hiyo.
Alifafanua kuwa uendelezaji wa mifumo hiyo utawapa fursa wakulima kuweza kushiriki kikamilifu katika kilimo wakiwa na uhakika wa kupata mazao mengi kuweza kujitosheleza kwa chakula na kujiongezea kipato pamoja na kuboresha hifadhi ya mazingira hasa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
Washiriki kwa pamoja wamepitisha azimio linalotambua mchango wa mifumo ya asili ya kilimo na ufugaji na wametoa wito wa kubaini mifumo asili iliyopo nchini, kutathmini mchango wake na changamoto kwa lengo la kuiboresha na kuiendeleza.

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU BEI ZA VYAKULA MIKOANI



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIAWIZARA YA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA


TAARIFA KWA UMMA  KUHUSU BEI ZA VYAKULA MIKOANI


UTANGULIZI: 

Tulianza msimu huu 2012/13 tukiwa na ziada kidogo ya chakula na kwa kujitosheleza kwa asilimia 113. Msimu huu, tofauti na msimu uliopita hatukuzuia wakulima na wafanyabiashara kuuza mazao yao nje ya nchi.

Pamoja na uzalishaji tuliokuwa nao katika maeneo kadhaa ya nchi kulikuwepo na maeneo ambayo uzalishaji wake haukuwa wa kuridhisha kutokana na hali mbaya ya hewa na hivyo kuwa na upungufu wa chakula.  Upungufu huu unajidhihirisha kutokana na kupungua  kwa uingiaji na upatikanaji wa vyakula sokoni, hususani unga wa mahindi ambacho ni chakula kikuu        na  bei ya soko kupanda  sana kwa viwango vilivyo juu ya bei ya wastani nchini.

Uchambuzi wa bei za vyakula unaonesha kwamba bei ya wastani ya mahindi kitaifa ni shilingi 675 kwa kilo.  Aidha, bei ya mahindi katika masoko ya miji mkuu ya baadhi ya mikoa iko juu ya wastani.  Kwa mfano, bei ya Dar es Salaam tarehe 28 Novemba, 2012 ilifikia shilingi 750 kwa kilo, Mwanza shilingi 825, Moshi shilingi 700, Tanga shilingi 785, Tabora shilingi 750 na Mtwara shilingi 735.  Aidha, unga wa sembe uliuzwa kati ya shilingi 1,100 na shilingi 1,500 kwa kilo, mwezi Desemba 2012.

Hali ilivyo katika maeneo mengi ya nchi ni kwamba, viwango vya upatikanaji wa chakula vinatofautiana katika maeneo mbali mbali.  Wakati mikoa minane (8) ya Iringa, Rukwa, Mbeya, Kagera, Mtwara, Kigoma, Ruvuma na Morogoro ilikuwa na ziada ya chakula, mikoa saba (7) ya Pwani, Mara, Tanga, Lindi, Mwanza, Singida na Dodoma ilikuwa na hali ya utoshelevu tu na mikoa sita (6) ya Shinyanga, Tabora, Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Dar es Salaam ilikuwa na uhaba wa chakula.

Kutokana na upungufu wa chakula kuzidi kujitokeza, mwezi Oktoba, 2012, Serikali, kupitia Kamati ya Maafa iliidhinisha mgao wa tani 18,417.8 wa chakula cha njaa kutoka katika maghala ya Hifadhi ya Chakula ya Taifa (National Food Reserve Agency) kwenda katika Halmashauri 35 za mikoa 12 zilizobainika kuwa na upungufu mkubwa wa chakula.  Mikoa iliyopewa chakula cha njaa ni Arusha, Dodoma, Kilimanjaro, Lindi, Mara, Manyara, Morogoro, Mwanza, Shinyanga, Singida, Tabora na Tanga.

Kutokana na hali ya upungufu wa chakula kuzidi kuendelea na kujitokeza kwa majanga mengine kama mafuriko, Serikali iliidhinisha mgao wa nyongeza ya chakula hadi kufikia tani 26,958.300 kwa Halmashauri zilizokuwa  na mahitaji makubwa ya chakula cha msaada.  Aidha, upungufu wa chakula katika baadhi ya maeneo yanayozalisha nafaka kwa wingi umesababisha kupungua kwa chakula kinachosambazwa katika soko hivyo kufanya usambazaji wa chakula kutolingana na mahitaji ya soko. Hali hii imesababisha kupanda kwa bei ya mahindi na unga wa  mahindi katika baadhi ya masoko hususan  ya mijini. Ili kukabiliana na hali hiyo Serikali imechukua  hatua zifuatazo:-
(i)      Kutoa chakula cha msaada kwa maeneo yaliyokuwa na upungufu wa chakula.
Kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu wenye upungufu wa chakula Serikali iliendelea kuongeza mgao wa chakula cha msaada kutoka tani 18,417.8 hadi kufikia  tani 28,250.300. Hadi kufikia mwezi Januari, 2013 jumla ya tani 19,040.865 za mahindi zilishachukuliwa. Aidha, jumla ya tani 9,209.435 bado hazijachukuliwa na mikoa iliiyopewa mgao wa nyongeza. Mikoa ambayo bado haijachukua nyongeza hiyo ni Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Tabora, Mbeya na Mara. Kiambatisho Na. 1
(ii)    Kuuza tani 40,000 za mahindi kutoka kwenye ghala la Taifa kwa ajili ya kushusha bei ya unga wa mahindi.

Serikali imeidhinisha kuuzwa tani 40,000 za mahindi kutoka katika ghala la chakula la taifa ambapo tani 20,000 zitauzwa kati ya mwezi Januari na Februari, 2013. Kwa bei ya shilingi 450 tu kwa kilo. Kiasi kingine cha tani 20,000 kilichobaki kitauzwa kuanzia mwezi Machi katika maeneo yatakayobainika kuwa na upungufu wa chakula na bei kuendelea kupanda. Mgao Kimkoa ni kama inavyoonyesha kwenye Kiambatisho Na. 2.

2.        UTARATIBU WA KUUZA MAHINDI KWA WASAGISHAJI
Mikoa yenye bei ya mahindi iliyo juu ya bei ya wastani kitaifa ndiyo iliyopewa mgao. Mikoa hiyo na mgao wake katika mabano ni kama ifuatavyo:  Arusha (tani 1100), Dodoma (tani 400), Kilimanjaro (tani 400), Lindi (tani 400), Mara (tani 900) , Manyara (tani 800), Morogoro (tani 400), Mwanza (tani 2500), Shinyanga (tani 1029), Singida (tani 500), Tabora (tani 1000), Tanga (tani 700), Mtwara (tani 600) , Pwani (tani 700), Simiyu (tani 1971) na Dar es Salaam (tani 6400).
Utaratibu unaotumika kuuza mahindi kwa wasagishaji ni kama ifuatavyo:
  i.        Mikoa imeelekezwa kuteua wasagishaji waaminifu wenye nia na uwezo wa kusagisha unga kwa ajili ya kuuza kwa walaji kwa bei elekezi iliyopangwa na mkoa ambayo ni kati ya shilingi 750 hadi 900 kwa kuzingatia gharama za usafirishaji.
 ii.        Wasagishaji walioteuliwa wanatakiwa kukidhi vigezo vilivyowekwa kama vile, uwezo wa kulipa fedha za mahindi ndani ya muda uliopangwa, uwezo wa kuhifadhi kiasi cha mahindi anachonunua, uwezo wa kusagisha, kufungasha na kusambaza unga ndani ya siku saba kuanzia siku aliyochukua mahindi, pamoja na kukubali kuuza kwa bei elekezi.
iii.        Wasagishaji walioteuliwa na mikoa watapewa vibali na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula ili waweze kununua mahindi kutoka katika maghala ya Wakala kama watakavyopangiwa.
iv.        Mikoa itaingia mikataba na wasagishaji walioteuliwa na kusimamia utekelezaji wa mikataba hiyo ili kuhakikisha mpango huu unatekelezwa kwa ufanisi na unaleta manufaa yaliyokusudiwa.


v.        Mikoa itachukua hatua kwa msagishaji ambaye atabainika kutumia vibaya kibali alichopewa, kama vile kuuza kibali hicho kwa msagishaji mwingine, kusafirisha na kuuza mahindi au unga kwenye maeneo tofauti na aliyopangiwa, kutosagisha na kuuza unga ndani ya siku saba kwa mujibu wa mkataba.
3.   UTEKELEZAJI WA MPANGO WA KUPUNGUZA BEI YA UNGA KWA WALAJI
Mikoa iliyopewa mgao imeelekezwa utaratibu wa kununua mahindi kutoka katika maghala ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula. Hadi kufikia tarehe 14 Januari, 2013 jumla ya mikoa 11 kati ya Mikoa 16 ilikuwa imewaslisha orodha ya wasagishaji kwa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula. Mikoa hiyo ni Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Singida, Dodoma, Morogoro, Lindi, Mtwara, Pwani,Tanga na Dar es Salaam. Mikoa ambayo haijawasilisha orodha ya wasagishaji ni Mwanza, Tabora, Shinyanga, Mara. 

Kuendelea kuchelewa kuwasilisha orodha ya wasagishaji kunasababisha kuchelewesha zoezi zima la utoaji wa mahindi, usafirishaji, usagishaji na hivyo kuchelewesha unga kuingia sokoni hali inayosababisha bei kuendelea kupanda.  Mikoa hiyo inaagizwa kuwasilisha orodha ya wasagishaji ndani ya siku saba kuanzia sasa.  Jumla ya wasagishaji 127 tayari wameshapewa vibali vya kununua mahindi yanayofikia tani 12,520.00 ambapo tani 7,858.291 zimeshalipiwa na uchukuaji unaendelea lakini kasi ya kulipia na kuchukua ni ndogo. Orodha ya Wasagishaji kama ilivyowasilishwa na mikoa na kiasi walichoidhinishiwa kununua imeoneshwa katika Kiambatisho Na.3.

Serikali inawaagiza Wasagishaji wote waliopewa vibali vya kununulia mahindi kuhakikisha wanalipia na kuchukua kiasi chote cha mahindi kama walivyoidhinishiwa katika vibali vyao ndani ya siku saba kuanzia sasa, vinginevyo Serikali italazimika kufuta vibali hivyo na kuvigawa upya kwa Wasagishaji wengine katika mikoa husika wenye nia thabiti ya kufikisha unga sokoni.
4.  USIMAMIZI NA UFUATILIAJI WA UTEKELEZAJI
Wakuu wa Mikoa  na Wilaya wanaagizwa kusimamia na kufuatilia kikamilifu utekelezaji wa zoezi hili kama ilivyoelekezwa. Aidha, mikoa inatakiwa kuweka mfumo mzuri wa usimamizi na usambazaji wa unga unaotokana na mahindi yaliyonunuliwa kutoka katika ghala la Serikali ikiwa ni pamoja na kuwafahamisha wananchi maeneo ambayo unga huo unapatikana pamoja na bei elekezi iliyopangwa na mikoa.
Katika ngazi ya Taifa Serikali, kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu imeandaa utaratibu wa kufuatilia utekelezaji wa mkakati huu katika mikoa yote iliyopata mgao wa chakula cha njaa au mgao ulitolewa kwa wasagishaji kwa ajili ya kupunguza bei ya unga katika masoko ya mijini.
5. MWISHO
Kwa kuwa maghala ya Dar es Salaam (Kipawa), Arusha, Dodoma na Shinyanga yana upungufu wa akiba ya chakula kulinganisha na mahitaji ya sasa katika maeneo hayo,  Serikali inaendelea kuhamisha chakula kutoka katika maghala yenye akiba ya kutosha kwenda katika maghala yenye upungufu ili kurahisisha usambazaji wa chakula katika maeneo yenye upungufu. Tunaendesha zoezi hili la kuhamisha  chakula kwa kutumia Shirika la Reli (TRL) , Jeshi la Wananchi na wasafirishaji binafsi ili kuhakikisha kwamba chakula kinafika haraka.

Tuesday, October 16, 2012

AGRICULTURE AND ENTERPRISES SKILLS FOR WOMEN SMALLHOLDERS PROJECT BY FASO


Women on their farms

Women now make up the majority of the agricultural sector in Tanzania, but recent evidence suggests that not only is their productivity constrained by a lack of appropriate skills training , but also that they are particularly vulnerable to a range of changes including economic and environmental changes. Equipping women on small farms with the skills to improve production and manage change is therefore an important step towards securing livelihoods and reducing poverty. Lack of credit and capital, insecure land tenure and inadequate rural infrastructure make the application of new agricultural and enterprise strategies risky for women smallholders. FASO can play an important role in mitigating these risks by facilitating access to credit, helping women manage capital, working towards more secure land tenure, and helping women lobby local government for the provision of better infrastructure.Training is best approach FASO will use to empower women in agriculture and enterprises development. Those skills will base on:-



Training in financial management
To run their businesses successfully, the women needed to be able to control and plan their finances. To do this, they needed to be able to price their goods, work out their profit margins, and understand when they were making a profit. The ability to price inputs (including the cost of labour), establish market prices, and understand the difference between income and profits, are important. FASO found that there important to deliver training designed to enable women, individually or in groups, to improve the financial management of their production: Training helps women to distinguish between personal money and business finances – individuals can take loans from business. They learn to make sure their debtors are not too many, to find reliable sources of credit, to manage their stock flows, and simple booking to manage their cash flows.

Training in marketing, packaging and pricing
In addition to financial management, smallholders also require marketing training. This was frequently noted in the interviews as one of the women’s most important concerns, well ahead of technical skills. Improving production techniques, although important, is not sufficient to create significant changes in their circumstances. Achieving more efficient production and increasing yields did not address one of the most serious problems for small producers, and especially women smallholders: their lack of market power. Problems with accessing markets forced women to sell their goods on disadvantageous terms, and prevented women reaping the full benefits of their work.

Training to support group organization
The appropriate training FASO will provide can support group organization. Groups need training and support at various points in their development in order to function effectively, and to have a chance to become self sufficient. FASO found that their groups had very similar needs in this area of:
  1. Training and guidance for group formation;
  2. Training in formulating constitutions and by-laws, decision making procedures and electing leaders, to enable the transparent regulation of the group; and
  3. Training in conflict management and leadership skills.
Training and guidance for group formation
The projects emphasized that groups that formed for the purposes of mutual support, as opposed to simply accessing credit, were more likely to operate successfully and have a better chance of ultimately becoming sustainable. Mostly of women started groups for three main reasons: socializing, access to savings and insurance, and changing practices and production

Training on access of credit in groups
A group approach (such as VICOBA) ensures that there is a collective responsibility for loans and reduces the individual risks. Project can play a valuable role in facilitating credit access for groups. It is important, however, that the initiative and responsibility for ensuring repayment remains with the group, as this is a key factor in ensuring the sustainability of credit access beyond the lifetime of a project. FASO Project will help groups to become more credit worthy by supporting proper group formation, and providing bookkeeping and literacy support.
FASO VICOBA Group training at Magereza, Moshi.

Training to enable transparent regulation of the group
The organizational training greatly improved the operation of the groups, and enabled them to make better use of their resources. Training in group management processes, such as establishing group regulations, leadership structures, and decision-making procedures, improved accountability within the group and reduced the potential for conflict between the executive and other members.

Training in conflict management and leadership skills
Training in how to discuss difficult topics with members and deal with challenging situations made the groups more stable and resilient, and therefore better able to achieve their goals over the long periods of time required.

 Benefits of enterprise training
The training can play an important role in helping prospective entrepreneurs become successful. For women, training in enterprise skills Is particularly valuable as they expanded into new areas. The entrepreneurship training is important in allowing producers in growth industries (including agriculture) to access more of the value chain associated with their product.
Women demanded a range of enterprise skills including bookkeeping, entrepreneurship and business management skills.
Developing the capacity of women and groups to take small, measured risks was both a major focus and a key challenge for each of the projects. While affecting this kind of change takes time, each project played an important role as a catalyst for this change.

IF YOUR A STAKEHOLDER ON AGRICULTURE, ENTERPRISES DEVELOPMENT, WOMEN EMPOWERMENT, etc CONTACT US FOR PARTNERSHIP TO IMPLEMENT THIS PROJECT..TOGETHER WE CAN!




Thursday, August 16, 2012

ROMANA MAKATA A STRONG WOMEN IN MOSHI.

FASO through a WED Program- Women Empowerment Development visited a strong women at Majengo street here in Moshi munispal. Romana is a aged women about 50 years who living with HIV. She is a widow, living in her own house at majengo street in moshi, a mudhouse but she trying to moderate her house by building a block house outside her mady house.

A women is an entrepreneur who practice horticulture, livestoking, cloth making 'Batiki'  and also she doing a food processing through drying. 'My source of income is through this activities and i built this house, paying fees for my child studying university, i used to get credits from majengo VICOBA and other financial institutions which help to increase my capital and sending my childrens and groundchildren to school and university '- she said.

'I need a support from government, non-goverment, individual and companies to help me so as i can live a better life through entreprenuership'

Romana in her trees plantation.

Romana show animal food she used to process

She is also a craftwomen

Romana show her chickens


She also selling a wood for source of power

She also doing urban farming

This is a house she build

A block house she build outside with a mudhouse in side she living.


She also packaging a medical seeds

Apart from that Roman own her registered enterprise called ADERMANA ENTERPRISES dealing with Batic processing and Handcraft. If you  want to contact with her just call her direct through phone number
+255 755 752 504 or contact as for more details.

Sunday, August 12, 2012

SHIRIKA LA FASO LAFANYA SEMINA YA KILIMO KWA VIJANA KATIKA KATA YA KAHE,MOSHI VIJIJINI.

 Shirika lisilo la kiserikari la Fumbuka Agro Solution Organization (FASO) limefanya semina ya kilimo kwa vijana wa kata ya kahe moshi vijijini siku ya jumamosi, tarehe 11/08/2012. Katika semina hiyo jumla ya vijana therathini (30) kutoka vijiji 6 (kila kijiji vijana 5), vijiji hivyo ni Ngasinyi,Oria,Mawalla,Mwangaria,Kisangesangeni na Rau waliudhulia semina hiyo ya mafunzo. Akizindua semina hiyo Diwani wa kata ya Kahe Mh.Aminiel Kimati amewataka vijana kufanya kazi na kuwa wavumilivu kusubili mafanikio bila kuwa na haraka. Diwani huyo amewataka vijana waudhulie katika semina mbalimbali za maendeleo na waache tabia ya kudai posho katika semina hizo kwani semina hizo ni kwa ajili ya maendeleo yao.

Afisa kilimo na mifugo wa kata ya Kahe Bw.Lekule amewataka vijana hao kufanya kitu cha ziada baada ya semina hiyo badala ya kusikiliza na kuacha mambo hayo waliyojifunza yaishie hewani. Mkufunzi wa semina hiyo Mwl.Mushi kutoka chuo cha Kilimo na Mifugo Mwangaria aliwafundisha vijana hao jinsi ya kuchagua mazao bora kulingana na hali ya hewa ya ukanda wao. Vile vile mkufunzi huyo aliwafundisha vijana hao jinsi ya kuchagua pembejeo bora za kilimo kama mbegu, mbolea na madawa ya kuulia wadudu.

Mkurugenzi wa FASO Bw.Innocent Mbele na Meneja miradi Ndg. Moringe Allayana kwa pamoja wamewataka vijana hao kuzingatia mbinu bora za kilimo na kuacha kulima kwa mazoea. Vilevile watendaji hao wa shirika la FASO wamewataka vijana hao wajiunge katika vikundi ili wafanye kazi kwa pamoja na kunufaika na fursa mbalimbali.

Washiriki wa semina hiyo wameonyesha kufurahishwa kwa kufanyika kwa semina hiyo na wameliomba shirika la FASO kuandaa semina nyingine kama hiyo katika kata ya kahe na vitongoji vyake.


Afisa Maendeleo ya jamii kata ya kahe akimkaribisha mgeni rasmi.



Diwani wa kata ya Kahe, Mh. Aminiel Kimati (aliyesimama) akifungua semina hiyo.

 Afisa Kilimo na Mifugo Kata ya Kahe, Ndg.Lekule akiongea na wananchi.
Mwl. Mushi kutoka chuo cha Mwangaria akitoa elimu ya kilimo kwa vijana.

Mwl. Mushi akifundisha vijana.

Meneja miradi ya FASO, Ndg Moringe Allayana (kulia) na wanasemina wakifuatilia kwa makini.

Mwl.Mushi na Bw.Lekule wote kwa pamoja wakisisitiza jambo.

 Kijana wa Kahe akiuliza swali katika semina hiyo.
Mkurugenzi mtendaji wa FASO, Bw.Mbele akinukuhu mambo mbalimbali katika semina hiyo.

Vijana wakifuatilia kwa makini semina hiyo.


Mkurugenzi mtendaji wa FASO, Bw.Mbele (aliyechuchumaa mwisho kulia) akiwa na wana semina.

 Meneja miradi ya FASO, Bw. Moringe Allayana (aliyechuchumaa mwisho kulia) akiwa na wanasemina
Afisa Kilimo wa kata ya kahe Ndg Lekule (kushoto), Kijana wa Kahe, Mwl. Mushi na Bw.Mbele (kulia)wakiwa katika picha ya pamoja

Friday, August 3, 2012

FASO YATEMBELEA CHUO CHA KILIMO NA UFUGAJI MWANGARIA.

 Katika harakati zake za kupunguza umaskini kwa kuimiza kilimo na ujasiriamali, shirika la FASO limetembelea chuo cha kilimo na ufugaji cha MWANGARIA kilichopo kata ya KAHE,Moshi Tanzania.Lengo la ziara hiyo lilikuwa kujenga mahusiano kati ya shirika la FASO na chuo hicho. Mahusiano hayo yamezaa matunda kwa kuanza kuandaa semina ya mafunzo kwa vijana katika kata ya KAHE.

Meneja miradi ya FASO, Ndg .Moringe akipeana mkono na mkuu wa chuo hicho, Mzee Ngitiama

Mkurugenzi mtendaji wa FASO,Bw.Mbele akipeana mkono na mkuu wa chuo hicho cha kilimo, Mzee Ngitiama.

Baadhi ya madarasa ya chuo hicho.