Friday, October 31, 2014

WAKULIMA KAHE WANUFAIKA NA MRADI WA MAHARAGE MACHANGA (FRENCH BEANS)

Shirika la FASO likishirikiana na mashirika mengine yani VECO TANZANIA na kampuni ya Frigoken yenye makao makuu yake nchini kenya, wamewawezesha wakulima wa kata ya Kahe kwa mara ya kwanza kulima maharage machanga.

Chini ya utaratibu wa kuwakopesha wakulima mbegu na vifaa vingine (k.m pembejeo) wakulima wa Kahe waliweza kuingia mkataba na kampuni ya Frigoken chini ya usimamizi wa shirika la FASO na VECO.

Wakulima hao wengi wao wakiwa vijana wameweza kunufaika kulima maharage machanga na kuiuzia kampuni ya Frigoken kulingana na mkataba waliojiwekea. ''Hii ni hatua nyingine ya maendeleo kwa mkulima mdogo kupata fursa ya kukupesheka pembejeo na kupatiwa soko, alisema Ndugu Elasto Mlayi, mkulima kiongozi wa kahe''.

 Wakulima wakikagua mazao yao
 Wakulima wakiwa kavuna maharage machanga

Wanunuzi wakiandaa vifaa tayari kununua maharage machanga kwa wakulima




Saturday, September 13, 2014

WAKULIMA WAPATIWA MAFUNZO YA USINDIKAJI


Shirika la FASO chini ya ufadhiri wa shirika la ILO kupitia The Foundation for Civil Society wametoa mafunzo ya usindikaji kwa wakulima katika kata ya KAHE. Huu ni mwendelezo wa mradi wa kuelimisha wakulima vijana juu ya kilimo cha mbogamboga, na usindikaji. Katika mafunzo hayo wakulima wapatao therasini walipatiwa mafunzo hayo kwa lengo la kuanza usindikaji lasmi kupitia chama chao cha KAHOCOSO. Mafunzo hayo yaliwezeshwa na Afisa Kilimo Moshi vijijini, (Horticulture) Bi. Mercy Urio na Bi. Modesta Mosha kutoka shirika la SIDO.


Afisa Kilimo Moshi(V) akiwa katika maandalizi ya somo la usindikaji.




Calvin Salema (Mwasibu wa Mradi-FASO) akishiriki katika maandalizi ya somo la usindikaji.


Nyaya zilizolimwa na wakulima hao tayari kwa usindikaji.


Maandalizi ya usindikaji yakiendelea.


Calvin Salema, mhasibu wa FASO akishiriki katika usindikaji


Wakulima wakichemsha nyanya tayari kwa usindikaji.


Mbogamboga zilizoandaliwa kwaajili ya usindikaji




Kifaa cha ukaushaji (solar dryer) kilichotumika katika ukaushaji wa mbogamboga.
M
Mbogamboga zikiandaliwa kwa ajili ya usindikaji.
Mboga mboga zikiweka katika solar dryer tayari kwa ukaushaji.


Mbogamboga zikiwekwa katika Solar dryer.


Nyanya zilizosindikwa zikiwekwa katika chupa tayari kwa matumizi.


Wakulima wakiifadhi nyanya zilizosindikwa tayari kwa matumizi


Madhumuni
Madhumuni ya semina hii ni uwawezesha wanakozi washiriki kuelewa sheria na kanuni za msingi katika kusindika vyakula.
  1.  Kuweza kutambua vifaa vinavyofaa
  2. Kuweka kuelewa usafi na mpangilio wa kiwanda
  3. Kuelezea matatizo yanayoweza kutokea kwa walaji kama usafi na usalama hauzingatiwi katika utengenezaji vyakul
  4. Kuweza kuorodhesha kanuni zausalama na kutengeneza vyakula bora
Mwezeshaji alisisitiza Kazi za kufungasha ni pamoja na kulinda chakula kutokana na:-
  1. ·         Kupoteza au kuchukua unyevu
  2. ·         Kupoteza hewa ya “carbon dioxide”
  3. ·         Kuchukua hewa ya ‘oxygen’
  4. ·         Uchafu, vumbi, udongo n.k
  5. ·         Kusagika, kupondeka n.k
  6. ·         Joto
  7. ·         Chembechembe wasiotakiwa/waharibifu
  8. ·         Wadudu, ndege na panya
  9. ·         Kupoteza au kuchukua harufu
  10. ·         Kuzuia mafuta n.k
Ufungashaji (Packaging)
Mwezeshaji vilevile alisisitiza kuwa katika uuzaji vyakula katika soko, ufungaji una umuhimu mkubwa katika maeneo ya mijini, kwenye ushindani mkubwa wa kuuza bidhaa, ufungashaji mzuri unatakiwa. Vyombo vinavyotumiwa kufungasha lazima view na maombo mazuri na ujazo ambao soko linataka.
Pia lebo ziwe zenye rangi na mpangilio wa kuvutia, pamoja na vielelezo vya kutosha kukidhi sheria za udhibit wa vyakula, Kama vile bei, anwani ya msindikaji, vilivyomo na tarehe za kutengeneza/kutumia bila kuharibika.
Mahita ya kufungasha vizuri yanaweza kuwa kazi kubwa kwa wazalishaji wadogo, maana gharama zake ni kubwa. Hata hivyo, kufungasha kukidhi matakwa ya walaji na sheria ya nchi ni muhimu. Vifungashio viko aina nyingi lakini vinavyotumiwa sana kufungasha vyakula vilivyosindikwa ni kama vifuatavyo:
  1. ·         Chupa na vyombo vya kioo
  2. ·         Chupa na vyombo vya plastic
  3. ·         Vyombo vya aluminium
  4. ·         Makopo na galoni za bati
  5. ·         Mifuko ya karatasi na plastic
  6. ·         Makasha ya karatasi
Miundo mbalimbali ya vyombo hivi inakidhi mahitaji mbalimbali kutegemea sifa za chakula na matakwa ya soko.
Kadhalika mifuko ya ‘plastic’, karatasi, ‘aluminium’ n.k. kutumiwa kufungasha vyakula mbalimbali kama vile vya maji na unga.
Makasha na maboksi ya uwezo mbalimbali yananunuliwa kufungasha bidhaa kwa soko la reja na jumla.

Monday, July 14, 2014

FASO EMPOWERING CHILDREN FROM FARMING FAMILY THROUGH ICT

THROUGH EMPOWERMENT OF FARMERS LIVES, FASO STARTED AN INITIATIVES OF TRAINING CHILDREN FROM FARMING FAMILY. BY SUPPORT FROM GERMANY ORGANIZATION CALLED LABDOO WHO PROVIDED USED LAPTOPS AND WORLD UNITE ORGANIZATION WHO BRING SUPPORTIVE VOLUNTEERS FROM DIFFERENT COUNTRIES, FASO TRAINING CHILDREN ON BASIC USES OF COMPUTER LIKE LATTER WRITING, DATA STORING ETC.


Children have a  porridge  during computer training

Children enjoy computer training

Frank Bubeck volunteer from Germany show a pupil laptop keyboard during training


Jacky(FASO staff) training children

Frank Bubeck with Abdi starting the journey to schools for computer training






Friday, June 27, 2014

WAKULIMA WAFUNDISHWA JINSI YA KUANDAA UDONGO WA KITALU

Shirika la FASO likishirikiana na mtaalamu wa kilimo kutoka shirika la TAHA wametoa elimu kwa wakulima wa kijiji cha Ngasinyi, Moshi vijijini. Katika elimu hiyo Afisa kilimo kutoka shirika la TAHA, ndugu Gilliard alitoa elimu ya kuandaa udongo kwa kuuchoma udongo ili kupunguza wadudu.  Elimu hiyo itawawezesha wakulima kutotumia dawa za kemikali katika kukabiliana na wadudu. Hatua hiyo ni mwanzo wa shamba darasa la nyanya litakalo andaliwa kwapamoja.

Wakulima wakiandaa udongo kwa ajili ya kitalu.


Udongo ukichemshwa ili kuua wadudu.

Wakulima wakishuhudia udongo unavyochomwa

Afisa kilimo kutoka TAHA, Ndg Gilliard akikoroga udongo


Udongo ukipakuliwa teyari kwa kuanza kutumika

Afisa kilimo akiupooza udongo uliochomwa.

Thursday, June 26, 2014

WAKULIMA WAPATIWA MAFUNZO YA KILIMO HAI


Wakulima wa kata ya Kahe, Moshi vijijini wapatiwa mafunzo ya kilimo hai chini ya mradi unaofadhiliwa na shirika la Thefoundation for Civil Society na ILO na kutekelezwa na shirika la FASO lenye makazi yake Moshi, Kilimanjaro-Tanzania.  Mafunzo hayo yalitolewa na mwezeshaji kutoka shirika la FROLESTA Bi. Fatuma. 



Bi. Fatuma, mwezeshaji kutoka shirika la FROLESTA akifundisha somo la kilimo hai kwa wakulima wa Kahe



Ndugu. Calvin Salema kutoka FASO akizungumza na wakulima wakati wa semina ya Kilimo hai.



Shamba darasa la kutengeneza mbolea ya mboji

Tuesday, October 8, 2013

YOUTH FARMERS TRAINED ON ENTREPRENEURSHIP IN KAHE WARD


Facilitator noting something on board.





Young farmers listening careful to the facilitator

Mr. Mbele, project coordinator prepare some training documentations during training.

Mr Calvin Salema, FASO project accountant during seminar workshop..

Youth farmers are considered as backbone of the country. In Tanzania youth is currently the largest group in its history facing a number of critical life decisions. Their well being and health is profoundly important for agribusiness development.

In this context, FASO is implementing a project funded by ILO through The Foundation for Civil Society (FCS) to provide five-day entrepreneurship training to youth farmers in Kahe ward, Moshi Rural recently to assist them to set up their own business (formal farming business) and save them from unemployment.

As part of Organic farming project, the training involved ILO entrepreneurship training packages and the trainer was Mr. Martin Jeremiah (Qualified ILO SYB trainer). Through those training youth farmers were offered business and counseling in areas including business start-up, business planning, management, marketing, finance and customer care.
The endeavors will be made to facilitate those youth farmers for market identification and product development. FASO will contribute in building networking with available Microfinance Institutions (MFIs) to the entrepreneurs for access to finance to establish small scale enterprise.

“Promoting entrepreneurship to youth farmers is our main worry and objective,” says Innocent Mbele, the Coordinator of the project. He indicates that in the country, the lack of employment is a major challenge encountered by youth. Although agriculture is a backbone of Tanzania economy, there is a decreasing interest among youth in entering agricultural related fields due to the persistent perception of agriculture as an outdated field with minimal financial returns. Agriculture must be made ‘sexy’ and profitable to the youth, and entrepreneurship training to young farmers is a one of the solution…He said. 

Wednesday, July 31, 2013

FASO SIGNED A CONTRACT WITH THE FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY



Mr. Innocent Mbele, FASO Executive Director (left) and Mr. Calvin Salema, Project Accountant (right) showing signed contracts.




FASO signed a contract with the foundation for civil society (ILO partner). The contract was signed by Mr. Innocent Mbele, Executive Director and Mr. Calvin Salema, Project accountant. Amounting to a total value of TSHS.21,777,000/- of which ILO through the foundation for civil society will funds amount to TSH.16,217,000/- and own contribution from FASO amounts to TSH.5,560,000/-. 

Project will be implemented in a period of nine (9) months, with the aim of training youth farmers on organic vegetables and fruits farming and processing. The project will be implemented in Kahe ward, Moshi Rural, Kilimanjaro-Tanzania.
 The project have the following focus:-
  1. Training youth on how to start and improve their own business (SIYB, ILO entrepreneurship package) .
  2. Training youth on how to form and operate a cooperative society
  3. Training youth on organic vegetables and fruits farming.
  4. Training youth on how to process vegetables and fruits.

Thursday, July 25, 2013

BENKI YA DUNIA YAIPA CHANGAMOTO AFRIKA KUBORESHA MATUMIZI YA ARDHI KUONDOA UMASIKINI


Ripoti ya Benki hiyo iliyotolewa Julai 22, 2013  imeeleza kuwa ingawa nchi za Afrika ina karibu nusu ya eneo la ardhi nzuri  ambayo haijaendelezwa kwa kilimo, bara hilo limeshindwa  kuiendeleza ardhi hiyoinayokadiriwa kuwa hekta milioni  202 kujikwamua katika umaskini, kuleta maendeleo ya uchumi,kuongeza nafasi za kazi na kulleta mafanikio kwa jumla.
 
Ripoti hiyo inayoitwa  “Kutumia ardhi ya Afrika kwa mafanikio ya pamoja,”  inaeleza kuwa  nchi za Afrika najamii zake zinaweza kabisa kuondoa tatizo la uporaji wa ardhi, kuzalisha mazao ya chakula na kubadilisha  taratibu za usimamizi na umiliki  wa ardhi katika mwongo ujao.Afrika, Ripoti  hiyo imeeleza, ina kiwango kikukbwa cha umaskini ambapo asilimia  47.5 ya watu wake wana kipato chini ya  dola za Marekani $1.25 kwa siku..

“Licha ya kuwa na ardhi kubwa na utajiri wa madini, Afrika bado ni maskini ,”  anasema  Makhtar Diop, Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia kwa Afrika.
“Kuboresha usimamiaji wa ardhi ni muhimu kwa maendeleo ya haraka na kutoa nafasi  zaidi kwa waafrika , wakiwemo wanawake ambao ni asilimia 70 ya wakulima wa Afrika ambao wanakwazwa  kumiliki ardhi na sheria za kimila..Hali hii haikubaliki na lazima ibadilike ili waafrika waweze kunufaika na ardhi yao.”

Ripoti hiyo imeeleza kuwa zaidi ya asilimia 90 ya ardhi ya ardhi haijarasimishwa, hivyo kuwa na hatari kubwa ya uporaji na kuchukuliwa kwa malipo ya chini ya fidia.
 
Hata hivyo kumekuwa na matumaini ya maboresho  chini ya mipango inayoendelezwa katika nchi za   Ghana, Malawi, Msumbiji,, Tanzania, na Uganda ambapo  mpango wa kutumia  ardhi kwa mafanikio ya pamoja  unaweza kuleta mapinduzi  ya  uzalishaji wa kilimo na uporaji wa ardhi na  kuondoa umaskini wa kutupea Afrika..

Mpango wa kuleta mabadiliko

Ripoti hiyo inapendekeza kuwa Afrika inaweza kufanikiwa kuendeleza ardhi yake  katika kipindi cha muongo ujao kwa::

· Kuwa na mabadiliko  na uwekezaji kurasimisha ardhi  na  maeneo muhimu yanayomilikiwa na watu binafsi.  Kusimamia taratibu za umiliki za maeneo yaliyovamiwa  na kujengwa  bila mpangilio mijini ambapo wanaishi zaidi ya  watu asilimila 60 barani Afrika.

Kukabiliana na udhaifu wa utawala na rushwa katika mfumo wa  usimamizi wa ardhi katika nchi za Afrika ambao  kwa kawaida unapendelea wakubwa na kuathiri maslahi ya wananchi walio maskini. Serikali za Afrika kuwa na dhamira  ya kisiasa  kuhimiza  mabadiliko haya ya ardhi kuvutia raslimali na uwezekezaji wa jamii ya kimataifa. .

Ripoti  hiyo inasema kuwa mpango huo utagharimu  nchi za Afrika  na  washirika wa maendeleo , ikiwemo sekta bianfsi kiasi cha  dola za Marekani bilioni 4.5  katika kipindi cha miaka 10 kuleta mabadiliko ya sera na uwekezaji