Monday, July 9, 2012

FASO YAFANYA ZIARA KUTEMBELEA WAKULIMA.


SHIRIKA LA FASO LIMEFANYA ZIARA KUTEMBELEA KIKUNDI CHA WAKULIMA "MSHIKAMANO GROUP" KINACHOFANYA SHUGHULI ZAKE MAENEO YA MSARANGA, MOSHI. KIKUNDI HICHO KINAJIHUSISHA NA KILIMO CHA MBOGAMBOGA NA KINAJUMUISHA WANACHAMA MBALIMBALI WENGIWAO WAKIWA VIJANA. LENGO LA ZIARA HIYO NI KUJENGA UKARIBU WA KIUTENDAJI KATI YA SHIRIKA NA WAKULIMA. VILE VILE KUTOA USHAURI NA KUJUA MATATIZO YANAYOWAKABILI WAKULIMA HAO WADOGO.
Mkurugenzi mtendaji wa shirika la FASO akikaguwa mifereji ya maji inayotumiwa na wakulima wa kikundi cha MSHIKAMANO















Meneja miradi ya FASO Bw.Moringe Allayana akiwa na wakulima wa MSHIKAMANO GROUP

FASO YATOA SEMINA KWA WAKAZI WA RAU.

Katika kuendeleza harakati za kuleta mabadiliko (hasa kiuchumi)  katika jamii FASO ilitoa semina fupi kwa wakazi wa kata ya RAU MADUKANI, Moshi mjini. Semina hiyo ilihusu kushawishi wananchi kujiunga katika vikundi vya kuweka na kukopoa (VICOBA). Semina ilifanyika katika mkutano wa hadhara wa kata ya RAU ulioitishwa na viongozi wa kata hiyo viwanja vya RAU madukani mjini Moshi..


 MKURUGENZI MTENDAJI WA FASO NDG. INNOCENT MBELE AKITOA SEMINA HIYO KWA WAKAZI WA RAU.
WAKAZI WA RAU KATIKA SEMINA YA VICOBA.

Friday, May 11, 2012

The United States African Development Foundation (USADF) provides a grant to Kongwa Cereal Growers Association

 Pictured are the Tanzania Country Program Coordinator of the U.S African Development foundation Godfrey Kassanga (left) presenting an official grant document to the Chairman of Kongwa Cereals Growers Association  Jeremiah Mwimbe Maina  (Third from right front row)during a grant signing ceremony held at USADF offices in Dar es Salaam on May 10, 2012. Witnessing the event were the USAID Trade and Investment Advisor Eric Johnson, Managing Director of Centre for Sustainable Development Initiative William Massawe (second from left) and some members and staff of CHAWANAKO.
CHAWANAKO's  Chairman Jeremiah Maina (Seated second from right) and Executive Secretary Jeremiah Mtagwa (centre seated)  signing on behalf of their association a grant document during a brief ceremony held at USADF offices in Dar es Salaam on May 10, 2012. Witnessing the event were the USAID Trade and Investment Advisor Eric Johnson (standing second from right), USADF Tanzania Country Program Coordinator Godfrey Kassanga (standing second from left) Managing Director of Centre for Sustainable Development Initiative William Massawe and some members and staff of CHAWANAKO.Photo courtesy of the American Embassy in Tanzania
---
The United States African Development Foundation (USADF) has provided a Tshs 116,575,000 (USD 100,000) grant to Kongwa Cereal Growers Association (CHAWANAKO) of Kongwa District in Dodoma to enable the Association implement its High Quality Food Grains Production and Marketing Project. The two years project aims at enhancing the association's prospects for sustainable food grains business expansion by supporting its more than 100 farmer members improve their cultivation and agronomy capacity.

Monday, April 16, 2012

Matumizi ya ardhi yashirikishe jamii

MIGOGORO ya ardhi imeendelea kuzikumba jamii nyingi katika maeneo mbalimbali nchini hivyo kusababisha migogoro.
Jamii inatumia muda mwingi kutatua migogoro hiyo badala ya kufanya shughuli za maendeleo.

Hali hiyo inatokana na ukweli kwamba, ardhi ndio tegemeo kubwa kwa jamii za wakulima na wafugaji ambao ndio sehemu kubwa ya Watanzania.

Ardhi ndio mtaji pekee ambao Watanzania wengi waishio vijijini wanaitegemea kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kuweza kuwapatia chakula na kipato.

Licha ya kuwepo kwa mamlaka zinazohusika na usimamizi pamoja na ugawaji wa ardhi, migogoro hiyo imeendelea kuwa sehemu ya maisha kwa jamii nyingi.

Kama sheria za usimamizi na umiliki wa ardhi zipo, kitu gani kinasababisha migogoro ambayo inagharimu maisha na mali za Watanzania wasio na hatia?

Sisi tunasema kuwa, sheria za ardhi zinatoa haki ya kutumia ardhi na si kuimiliki hivyo inatosha kumhakikishia mtu kuwa, kitu chochote ambacho atakiendeleza katika ardhi husika, kitalindwa kwa maslahi yake si lazima kumwambia ardhi hiyo ni yako ili aiendeleze.


Migogoro ya ardhi husababishwa na mambo mbalimbali ambayo baadhi yake ni upungufu katika sheria za ardhi, mamlaka zinazohusika na ugawaji wa viwanja kugawa kiwanja kimoja kwa mtu zaidi ya mmoja na fidia ndogo.

Licha ya kufanyika marekebisho katika sheria za kusimamia matumizi ya ardhi, bado migogoro hiyo imeendelea kuchukua nafasi miongoni mwa jamii nyingi za Kitanzania.

Upo umuhimu mkubwa wa kushirikisha jamii katika kufanya maamuzi yanayohusu matumizi ya ardhi. Kama wananchi watashirikishwa, migogoro mingi iliyopo vijiji itapungua.

Ipo tabia ya baadhi ya Halmashauri za vijiji, kupitisha taarifa feki inayoamua matumizi ya ardhi ya kijiji bila ridhaa ya wananchi.

Serikali nayo inachangia migogoro hii pale inaposhindwa kulipa fidia kwa wananchi baada ya kutwaa ardhi kwa ajili ya kufanikisha miradi mbalimbali ya maendeleo.

Umefika wakati wa wananchi kuelimishwa juu ya sheria mbalimbali za ardhi ili watambue haki na wajibu wao katika suala zima la umiliki na matumizi ya yake.

CHANZO; MAJIRA

Vijana watakiwa kujenga utamaduniwa wa kujitolea shughuli za maendeleo

VIJANA wametakiwa kujenga utamaduni wa kujitolea na kutoa michango katika shughuli mbalimbali za kijamii bila kusubiri kusukumwa kufanya hivyo.

Wito huo umetolewa na Meneja Masoko wa Chuo kikuu cha Dar es salaam(UDSM), Dk Omary Mbura alipokuwa akitoa mada katika warsha iliyowahusisha wanafunzi wa chuo hicho jana jijini.
Alisema , vijana hawana budi kutumia nguvu , jitihada na uwezo wao katika kuchangia shughuli za kijamii ili taifa linufaike kupitia wao kwa kuwa sehemu kubwa ya maendeleo ya nchi inategemea nguvu kazi ya vijana.

“Vijana ndiyo nguvu kazi ya taifa ni jukumu la kila mmoja wenu kwa nafasi yake kuhakikisha anachangia katika shughuli za kijamii, lengo ikiwa ni kuliletea maendeleo taifa ambalo kwa kiasi kikubwa linategemea utendaji kazi mzuri wa vijana”alisema Mbura

Aliongeza kuwa , sehemu kubwa ya vijana wanaomaliza katika chuo hicho wanaenda kuwa viongozi katika sekta mbalimbali hivyo hawana budi kutumia mafunzo waliyopata kuwa mfano bora katika kulilietea taifa maendeleo.

Naye Muhsin Masoud ambaye alikuwa mwezeshaji katika warsha hiyo alisema, wakati umefika sasa kwa vijana kubadilika na kufanya mambo ambayo kwa namna moja ama nyingine yatakuwa na mchango mkubwa kwa taifa.
Alisema vijana hawana budi kupingana na mmomnyoko wa maadili ambao unaonekana kushika hatamu kwa sasa na badala yake wazingatie maadili pamoja na kanuni ambazo hazina lengo la kupindisha sheria.
CHANZO: MWANANCHI
16th April 2012

Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Wadogo Tanzania (Mviwata) umeandaa kongamano la kitaifa ambalo pamoja na mambo mengine litajadili na kutoa tamko la kupinga mauaji ya wakulima wadogo nchini, wanaouawa katika harakati za kutetea ardhi yao.

Kongamano hilo linatarajiwa kufanyika mjini Morogoro kesho ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya siku ya Wakulima Wadogo Ulimwenguni, litajadili athari za uporaji wa ardhi kwa wazalishaji wadogo nchini.

Aprili 17 kila mwaka ni siku ya maadhimisho ya harakati za wakulima wadogo ulimwenguni. Maadhimisho hayo hufanyika ikiwa ni kumbukumbu ya mauaji ya wakulima wadogo 19 yaliyotokea nchini Brazil mwaka 1996 wakiwa katika harakati za kutetea haki yao na kuzuia uporaji wa ardhi waliyokuwa wakiitegemea kwa uzalishaji.

Mratibu wa maandalizi ya kongamano hilo, Thomas Laiser, alisema jana kuwa Mviwata imeandaa kongamano hilo ili kuzungumzia mustakabali wa wakulima wadogo Tanzania, ikiwemo mauaji ya wakulima yanayoendelea kutokea wakati wa harakati za kuwaondoa kwenye maeneo yao.

“Katika miaka ya karibuni nchini Tanzania tumeshuhudia kasi ya uporaji wa ardhi ya wazalishaji wadogo vijijini ikijumuisha matumizi ya nguvu kupita kiasi na hata mauaji jambo ambalo halitoi ishara njema ya hatma ya wakulima na wazalishaji wengine wadogo,” alisema Laiser ambaye pia ni Afisa Ushawishi na Utetezi wa mtandao huo.

Aliongeza kuwa “uhamishwaji kwa nguvu ili kupisha wawekezaji wa ndani na nje na wakati mwingine upanuzi wa ardhi za hifadhi, zimetajwa kuwa sababu za kuhalalisha vitendo hivyo ambavyo vimewaacha wazalishaji wengi wadogo katika baadhi ya maeneo wakiwa wamepoteza makazi, mali na maisha yao.”

Laiser alitolea mfano wa matukio ya kuwahamishwa kwa nguvu wafugaji katika bonde la Ihefu, hifadhi ya Loliondo, Malinyi Ulanga, Meatu, Kiteto na kwingineko nchini yakiwemo mauaji ya wakulima watano wilayani Ulanga siku za karibuni ni mfano wa adha ambazo wazalishaji wadogo wamekuwa wakikabiliana nazo kutokana na uporaji wa ardhi unaoendelea kufanyika.

Kongamano hilo pia litazijadili athari mahsusi zinazowakabili wanawake na watoto vijijini katika harakati za utwaaji ardhi na kutoa wito kwa viongozi wa kisiasa na serikali wa ngazi mbalimbali kuwalinda na kuisimamia haki ya ardhi ya wazalishaji wadogo vijijini.

Laiser alisema kongamano hilo litakuwa na washiriki zaidi ya 90 wakiwemo wakulima 70 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania kati yao theluthi mbili wakiwa ni wanawake.

Washiriki wengine kwenye kongamano hilo watakuwa ni wanahabari, waalikwa toka mashirika yanayotetea haki za ardhi nchini, wawakilishi wa taasisi zingine za kiraia, wanaharakati, wanataaluma na baadhi ya viongozi na wafanyakazi wa mtandao huo.

CHANZO: NIPASHE

UTUPA, MMEA WA AJABU UNAOUA WADUDU

Utupa (Tephrosia vogelii) ni mmea wa jamii ya mikunde ambao huishi kwa muda unaozidi miaka mitatu. Mmea huu hutoa maua mengi, kuzaa mbegu nyingi na una majani mengi. Mmea huu hukua haraka pia ni rahisi kuzalisha. Huweza kukua hadi kufikia urefu wa futi 10. Inashauriwa kuukata baada ya miaka mitatu ili kurefusha maisha yake na kuwezesha kutoa majani mengi. Mmea huu hustawi vizuri sehemu mbalimbali na zipo aina kuu tatu. Aina hizo zinatofautishwa kwa maua yake kama ifuatavyo: inayotoa maua ya njano, pinki na meupe.

Utupa unaoteshwa kwa mbegu na unakuwa tayari kutumika baada ya miezi 4-6 tangu mbegu zipandwe. Sehemu yenye sumu katika utupa ni majani na mizizi. Inadhuru visumbufu wa mimea vinapokula na kugusa, hii inavisababishia kukosa hamu ya kula.

Utupa unaweza kutumika kama kiuatilifu cha wadudu kama vile kupe, utitiri, kimamba, cabbage headworm, viwavi, sota funza wa vitumba, bungua wa mahindi, vithiripi, fuko, viroboto, chawa na magonjwa ya ngozi.

Pia utupa unafaa kutandaza shambani na kurutubisha ardhi.
Kutayarisha dawa ya majani ya utupa Kwa ajili ya kuua wadudu

Chuma majani mabichi kulingana na mahitaji ya shamba lako (hasa kabla mmea haujatoa mbegu kwani wakati huo dawa aina ya tephrosine ipo nyingi zaidi).

Yatwange mpaka yawe laini.

Loweka katika lita 20 za maji safi kwa muda wa masaa ishirini na nne katika uwiano wa 1:20 (kg 1 ya utupa kwenye lita 20 za maji).

Chuja mchanganyiko huo vizuri ili kuondoa vipande vya majani. Unaweza kutumia chujio la bomba.

Nyunyizia mboga zako au mimea mingine kama dawa nyingine. Tofauti iliyopo kati ya dawa hii na madawa ya kemikali ni kwamba haina harufu kali na madhara kwa afya ya mnyunyiziaji.

Dawa hii huweza kuua viwavi wa nyanya, nondo wa kabeji, wadudu mafuta na funza wa mabua ya mahindi (stalk borers), wadudu wanaoshambulia matango na kahawa.

Inapendekezwa itumike kabla mimea haijashambuliwa. Huua pia wadudu walao majani na mashina kama viwavi jeshi.

Unga unaotokana na majani ya utupa unaweza pia kutumika kuhifadhi nafaka hasa kwa ajili ya mbegu.
Kutayarisha dawa ya unga wa utupa

Twanga majani hadi yawe laini na uanike.

Saga majani yaliyotwangwa na kuanikwa kuwa unga.

Wakati wa kuotesha mazao, changanya unga wa dawa na mbegu ya zao unalotaka kupanda.

Tumia shambani kwa kunyunyizia dawa kwa kushika kwenye vidole vitatu kwa shina moja la kabichi.
Matumizi ya ghalani

Majani ya utupa yanatumika pia kuhifadhia mazao ghalani.

Yanatumika kufukuza fukuzi na mende wa maharage.

Chuma majani ya utupa, anika kwenye kivuli, twanga majani kupata unga.

Pima na changanya gm 100 katika kg 100 za nafaka/mikunde.

Dawa hii inatumika pia kuhifadhi mahindi.
Tahadhari kwa watumiaji

Kuvaa kinga ya mwili mzima wakati wa unyunyuziaji

Tumia dawa baada ya uchunguzi wa visumbufu

Usile mazao kabla ya siku 10- 14 kwisha baada ya kunyunyuzia dawa

Iwekwe mbali na watoto, maji na mifugo

Utupa ni sumu kali kwa samaki, inaweza kuua wadudu marafiki na wanyama.

Kwa nafaka za chakula hakikisha unga wa dawa unakaushwa vya kutosha kwani unaweza kusababisha harufu kali kwenye nafaka.

Wednesday, April 4, 2012

Challenges of Tanzanian green revolution movement

For more than four decades Tanzania has been struggling to spur economic growth and eliminate poverty. But by any standard achievement of this goal is not near sight. The Poverty and Human Development Report 2007, indicates that the proportion of the population that cannot meet their daily basic needs has declined by only 2.4 percent from 35.7 percent between 2001 and 2007. At the same time, the number of people living in poverty has increased by 1.0 million people from 11.7 million. Although poverty affects both urban and rural people, it is those living in the rural areas who are hit hard. This accentuates the notion that poverty is basically a rural phenomenon. Based on this trend the MKUKUTA and the Millennium Development Goal (MDG) target of reducing income poverty to 19% by 2010 and 2015 respectively will be missed.

This observation is an eye opener on the likely failure of whatever model pursued by government to achieve economic growth through agriculture. Asian countries, previously at equal footing with Tanzania have tremendously revolutionalised their agriculture and transformed their economies. Of recent, Malawi, a country with food deficit for several years is now with food surplus and even donating maize to neighbouring countries of Lesotho and Swaziland. Ethiopia is another good example in the making. The achievements of Malawi and Ethiopia have not happened by chance. It is a result of committed leadership that is willing to do the right things with the right magnitude on the right path to agricultural development. Both countries have already met the Comprehensive African Agricultural Development Programme (CAADP) target of allocating at least 10% of national budgets to agriculture. For example, in 2007 agriculture made up 12 percent of the national budget in Malawi and 11 percent in Ethiopia as compared to only 6.2 percent for Tanzania during the same year. This year the government has increased the proportion of agriculture in the national budget by only 0.7 percent to 6.9 percent, and has intensified propaganda to make the public feel that agriculture has now assumed first priority in government plans in what it termed “Kilimo Kwanza”.

In order to speed up the process of transforming agriculture in Tanzania, it is imperative to understand the context of the challenges facing farmers in the country while drawing lessons from those who have made it like India and Mexico or those who are on the route to success like Malawi and Ethiopia. Success of green revolution in a country like ours is hinged on the understanding that over 90 percent of agricultural output is produced by smallholder farmers scattered in rural communities all over the country. They spend hours and hours of backbreaking labour to produce very little from their farms because of numerous constraints facing them.

Well-thought plans are required to empower them. Prof. Sanchez who co-chairs the Hunger Task Force of the Millennium Project of the United Nations Millennium Development Goals observes that what rural African farmers need is empowerment. They need the right quantity and quality of fertilizer at the right time, credit support to enhance and expand their holdings, efficient crop processing capabilities to add value to farm produce, and good market outlets to sell their harvests. However, a critical observer would quickly sense that there is nothing new in Prof. Sanchez’s assertion. Between 2003/4 and 2008/9 the government of Tanzania spent TSh. 128.7 billions to subsidise 487,984 tons of fertiliser to smallholder farmers. Furthermore, during the same period Tanzania subsidised 1,071 tones of seeds and 13,700,000 seedlings to farmers; and through the District Agriculture Development Plans (DADPS) it has provided loan to farmers for buying 186 power tillers and allocated approximately 8 billions to irrigation. Whether all this money reaches beneficiaries and has resulted into improved agricultural productivity is a debatable issue.

Out of frustration one may ask; why then is green revolution taking too long to achieve in Tanzania? The answers to this questions lies in the fact that Tanzania hasn’t been lucky enough to have unequivocally committed person among policy makers who is willing to liberate farmers from the shackles of poverty. We can have beautiful plan to support agriculture and spend billions of money on those plans, but if we are lacking a person who is committed body and soul to see to it that changes really happen on the ground, not much would be realised. Such extra commitment is vital because not everything can be coded in the project documents. Those leading agricultural development programmes in Tanzania are people appointed on the criteria best known to the appointing authority; they have little to demonstrate their commitment and interest in agriculture.

The situation is different in the countries that have succeeded in green revolution. The success revolves around a person. The success of green revolution in Mexico is attributed to the then Mexican President, Ávila Comacho whose keen interest to move agriculture beyond subsistence farming, made him work out an agreement with the Rockefeller Foundation to carryout an intensive breeding program that resulted into wheat varieties that sparked the green revolution. In India the success is attributed to the then Minister of Agriculture, Dr. Monkombu Sambasivan Swaminathan who despite bureaucratic hurdles invited Dr. Norman Borlaug under the Ford Foundation to replicate the Mexican success. The success of the “white revolution” in India (an equivalent to green revolution in the livestock sector) is due to Dr. Verghese Kurien who architected the “Operation Flood” the largest dairy development programme in the world that saw India becoming the largest milk producer in the world. Lastly, the recent success of Malawian agriculture is credited to the Malawian President, Bingu wa Mutharika who appointed himself minister of agriculture in order to have direct supervision of agricultural development programs and ensure that their outputs and impacts are maximised. In the Tanzanian context whose commitment emulates the people mentioned above? The urge to transform agriculture is mere lip service. We should not forget that people do not eat words; concrete pragmatic plans are needed to translate those words into improved livelihood of the people especially those in the captivity of agriculture.

By Dr. Damian M. Gabagambi, SUA